-
Wenye Kufariji UnaokuhusuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.”—Isaya 41:8-10.
-
-
Wenye Kufariji UnaokuhusuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Watumishi wa Mungu hawatahitaji kutetemeka eti Koreshi mshindi anakuja. Yehova atakuwa pamoja na watu wake ili kuwasaidia.
14. Watumishi wa Mungu wanafarijiwaje leo na maneno ambayo Yehova aliambia Israeli?
14 Maneno hayo yamewapa watumishi wa Mungu uhakikisho na nguvu mpaka siku zetu. Kule nyuma mwaka wa 1918, wao walitaka sana kujua mapenzi ya Yehova kwao. Walitamani kukombolewa kutoka utekwa wao wa kiroho. Leo sisi tunatamani kupata kitulizo tutoke kwenye mikazo tunayotwikwa na Shetani, ulimwengu, na kutokamilika kwetu wenyewe. Lakini tunafahamu kwamba Yehova anajua wakati na jinsi hasa ya kusaidia watu wake. Kama watoto wadogo, sisi tunaendelea kushika mkono wake hodari, tukiwa na hakika atatusaidia kukabiliana na hali. (Zaburi 63:7, 8) Yehova huwathamini wanaomtumikia. Yeye hututegemeza sisi leo sawa na vile alivyowategemeza watu wake kupita katika kile kipindi kigumu cha mwaka wa 1918 mpaka wa 1919, na sawa na vile alivyowategemeza Waisraeli waaminifu zamani za kale.
-