-
Wenye Kufariji UnaokuhusuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
17, 18. Isaya anaelezaje juu ya kutiwa nguvu kwa Israeli, nasi tuwe na uhakikisho wa utimizo gani?
17 Yehova anaendelea kufariji watu wake: “Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno [“kuwili,” “NW”]; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi.
-
-
Wenye Kufariji UnaokuhusuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
18 Israeli atapewa nguvu ashambulie ili kujitetea, na kuwatiisha kiroho adui zake walio kama milima. Israeli arudipo kutoka uhamishoni, atawashinda maadui wanaojaribu kuzuia hekalu na kuta za Yerusalemu zisijengwe upya. (Ezra 6:12; Nehemia 6:16) Hata hivyo, maneno ya Yehova yatatimizwa kwa kadiri kubwa juu ya “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Yesu anawaahidi Wakristo watiwa-mafuta hivi: “Yeye ashindaye na kushika vitendo vyangu hadi mwisho hakika nitampa mamlaka juu ya mataifa, naye hakika atachunga watu kwa fimbo ya chuma hivi kwamba watavunjwa vipande-vipande kama vyombo vya udongo wa mfinyanzi, sawa na vile mimi nimepokea kutoka kwa Baba yangu.” (Ufunuo 2:26, 27) Hakika wakati utafika ambapo ndugu za Kristo waliofufuliwa kwenye utukufu wa kimbingu watashiriki kuwaangamiza adui za Yehova Mungu.—2 Wathesalonike 1:7, 8; Ufunuo 20:4, 6.
-