-
Wenye Kufariji UnaokuhusuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia BWANA, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli.”—Isaya 41:15, 16.
-
-
Wenye Kufariji UnaokuhusuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Israeli arudipo kutoka uhamishoni, atawashinda maadui wanaojaribu kuzuia hekalu na kuta za Yerusalemu zisijengwe upya. (Ezra 6:12; Nehemia 6:16) Hata hivyo, maneno ya Yehova yatatimizwa kwa kadiri kubwa juu ya “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Yesu anawaahidi Wakristo watiwa-mafuta hivi: “Yeye ashindaye na kushika vitendo vyangu hadi mwisho hakika nitampa mamlaka juu ya mataifa, naye hakika atachunga watu kwa fimbo ya chuma hivi kwamba watavunjwa vipande-vipande kama vyombo vya udongo wa mfinyanzi, sawa na vile mimi nimepokea kutoka kwa Baba yangu.” (Ufunuo 2:26, 27) Hakika wakati utafika ambapo ndugu za Kristo waliofufuliwa kwenye utukufu wa kimbingu watashiriki kuwaangamiza adui za Yehova Mungu.—2 Wathesalonike 1:7, 8; Ufunuo 20:4, 6.
-