-
“Ninyi Ni Mashahidi Wangu”!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.
-
-
“Ninyi Ni Mashahidi Wangu”!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Hata hivyo, sasa Yehova anataka watu wake wamtukuze kwa sababu ya “neno jipya”—jambo watakalojionea wenyewe. Linatia ndani si ukombozi wao kutoka Babiloni tu, bali pia safari yao ya kurudi kwao kimwujiza, labda kwa kufuata ile njia ya moja kwa moja ya jangwani. Katika nchi hiyo tasa, Yehova atawafanyia “njia,” awafanyie maajabu yatakayowakumbusha yale aliyowafanyia Waisraeli siku za Musa—ndiyo, awalishe jangwani hao wenye kurudi, azime kiu yao kwa mito ya hakika.
-
-
“Ninyi Ni Mashahidi Wangu”!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
19. Mabaki ya Israeli wa kiroho na waandamani wao wanatembeaje katika “Njia ya utakatifu”?
19 Vivyo hivyo, mwaka wa 1919 mabaki ya Israeli wa kiroho waliwekwa huru kutoka utekwa wa Kibabiloni, wakaanza safari kufuata njia waliyotayarishiwa na Yehova, “Njia ya utakatifu.” (Isaya 35:8) Haikuwa lazima wapitie jangwa lenye joto kali kama Waisraeli, kutoka hapa kwenda hapa, wala safari yao haikwisha baada ya miezi michache ya kufika mahali fulani Yerusalemu. Hata hivyo, “Njia ya utakatifu” iliwaongoza mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta kuingia katika paradiso ya kiroho. Nao hubaki katika “Njia ya utakatifu,” maana ni lazima bado waendelee na safari kuuvuka mfumo huu wa mambo. Mradi wanabaki katika ile njia kuu—mradi wanashika viwango vya Mungu vya usafi na utakatifu—wanabaki katika paradiso ya kiroho.
-