-
Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Basi, shamba hilo la mizabibu ni nini? Mmilikaji aeleza: “Shamba la mizabibu la BWANA wa majeshi ndilo nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni mche wake wa kupendeza.”—Isaya 5:7a.
-
-
Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
14. Yehova atarajia matunda gani kutoka kwa taifa lake, lakini hilo lazaa nini badala yake?
14 Mungu atarajia taifa hilo lizae matunda mema. Mika, aliyeishi wakati wa Isaya, atangaza hivi: “BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!” (Mika 6:8; Zekaria 7:9) Hata hivyo, taifa hilo lashindwa kutii himizo la Yehova. “[Mungu] akatumaini kuona hukumu ya haki, na kumbe! aliona dhuluma; alitumaini kuona haki, na kumbe! alisikia kilio.” (Isaya 5:7b) Musa alitabiri kuwa taifa hilo lisilo na uaminifu lingezaa zabibu zenye sumu kutoka kwa “mzabibu wa Sodoma.” (Kumbukumbu la Torati 32:32) Basi, yaelekea kwamba ukosefu wa adili katika ngono, pamoja na ugoni-jinsia-moja, ni sehemu ya mkengeuko wao kutoka kwa Sheria ya Mungu. (Mambo ya Walawi 18:22) Usemi “dhuluma [“uvunjaji wa sheria,” NW]” waweza pia kufasiriwa “umwagaji wa damu.” Hapana budi matendo hayo ya kinyama yamesababisha “kilio” kwa wale wanaotendwa vibaya—kilio ambacho kimeyafikia masikio ya Mpanzi wa shamba la mizabibu.—Linganisha Ayubu 34:28.
15, 16. Wakristo wa kweli waweza kuepukaje kuzaa matunda mabovu ambayo Israeli ilizaa?
15 Yehova Mungu “apenda uadilifu na haki.” (Zaburi 33:5, BHN) Aliwaamuru Wayahudi hivi: “Msitende yasiyo haki katika hukumu, usimpendelee mtu maskini, wala kumstahi mwenye nguvu; bali utamhukumu jirani yako kwa haki.” (Mambo ya Walawi 19:15) Kwa hiyo ni lazima tuepuke kuegemea upande mmoja tunaposhughulikiana, wala tusiruhusu kamwe mambo kama vile jamii, umri, mali, au umaskini yapotoe maoni yetu kuhusu watu. (Yakobo 2:1-4) Hasa ni muhimu kwa waangalizi ‘kutofanya jambo lolote kulingana na mwelekeo wenye kuegemea upande,’ sikuzote wajaribu kusikiliza pande zote za jambo kabla ya kukata hukumu.—1 Timotheo 5:21; Mithali 18:13.
-
-
Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Kutambua Shamba la Mizabibu la Mungu Leo
10. Yesu alitoa mfano gani unaohusu shamba la mizabibu?
10 Huenda Yesu alikuwa akizingatia maneno ya Isaya alipotoa mfano wa walimaji wauaji: “Kulikuwa na mtu, mwenye nyumba, aliyepanda shamba la mizabibu na kuweka ua kulizunguka naye akachimba sindikio la divai katika hilo akasimamisha mnara, na kulikodisha kwa walimaji, na kusafiri nchi ya nje.” Kwa kuhuzunisha, walimaji hao walimsaliti mmilikaji wa shamba hilo la mizabibu, hata wakamwua mwanaye. Kisha Yesu akaonyesha kuwa mfano huo ulihusisha mengi kuliko tu Israeli halisi, aliposema hivi: “Ufalme wa Mungu utachukuliwa kutoka kwenu [Israeli la kimwili] na kupewa kwa taifa lenye kutokeza matunda yao.”—Mathayo 21:33-41, 43.
11. Ni shamba gani la mizabibu la kiroho lililokuwapo katika karne ya kwanza, lakini ni nini kilichotukia baada ya kifo cha mitume?
11 “Taifa” jipya hilo lilithibitika kuwa “Israeli wa Mungu”—taifa la kiroho la Wakristo watiwa-mafuta lenye idadi ya jumla ya 144,000. (Wagalatia 6:16; 1 Petro 2:9, 10; Ufunuo 7:3, 4) Yesu aliwafananisha wanafunzi hao na “matawi” katika “mzabibu wa kweli,” yaani, yeye mwenyewe. Kwa kawaida, matawi hayo hutarajiwa kuzaa matunda. (Yohana 15:1-5) Ni lazima wadhihirishe sifa kama za Kristo na kuishiriki kazi ya kuhubiri “habari njema hii ya ufalme.” (Mathayo 24:14; Wagalatia 5:22, 23) Lakini tangu kifo cha wale mitume kumi na wawili, wengi wa wale wanaodai kuwa matawi ya “mzabibu wa kweli” wamethibitika kuwa bandia—kwa kuzaa zabibu-mwitu badala ya matunda mema.—Mathayo 13:24-30, 38, 39.
12. Maneno ya Isaya yahukumuje Jumuiya ya Wakristo, nayo yana fundisho gani kwa Wakristo wa kweli?
12 Kwa hiyo, shutuma ya Isaya juu ya Yuda yahusu Jumuiya ya Wakristo leo. Uchunguzi wa historia yake—vita zake, krusedi zake, Mabaraza yake ya Kuhukumu Wazushi—wafunua kadiri ambayo matunda yake yamekuwa machungu! Hata hivyo, shamba la mizabibu la kweli la Wakristo watiwa-mafuta pamoja na waandamani wao wa “umati mkubwa” lazima watii maneno ya Isaya. (Ufunuo 7:9) Iwapo watampendeza mmilikaji wa shamba la mizabibu, ni lazima wao, mmoja-mmoja na pia wakiwa kikundi, wazae matunda yanayompendeza.
-