Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova—“Mungu Mwenye Haki, Mwokozi”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sikusema kwa siri, katika mahali pa nchi ya giza; sikuwaambia wazao wa Yakobo; Nitafuteni bure; Mimi, BWANA, nasema haki; nanena mambo ya adili.” (Isaya 45:18, 19) Kwa mara ya nne na ya mwisho kabisa katika sura hii, Isaya anafungua kifungu cha maneno mazito ya unabii kwa usemi huu: ‘BWANA asema hivi.’ (Isaya 45:1, 11, 14)

  • Yehova—“Mungu Mwenye Haki, Mwokozi”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Hakuiumba dunia “bure.” Vivyo hivyo, yeye hawaombi watu wake, Israeli, wamtafute “bure.” Sawa na vile kusudi la Mungu kwa dunia litakavyotimizwa, ndivyo kusudi la Mungu kwa wateule wake litakavyotimizwa. Maneno ya Yehova husemwa waziwazi, tofauti na matamko yasiyo wazi ya wale wanaotumikia miungu ya uwongo. Maneno yake ni ya haki, nayo yatatimia. Wale wanaomtumikia hawatamtumikia bure tu.

      22. (a) Wayahudi waliopelekwa uhamishoni Babiloni wanaweza kuwa na uhakika wa jambo gani? (b) Wakristo leo wana uhakikisho gani?

      22 Maneno hayo yanawahakikishia watu wa Mungu waliopelekwa uhamishoni Babiloni kwamba Nchi ya Ahadi haitabaki ukiwa. Itakaliwa upya. Na ahadi za Yehova kuwahusu zinatimia. Kwa maana pana, maneno ya Isaya yanawahakikishia watu wa Mungu leo kwamba dunia haitakuwa magofu yenye ukiwa—ichomwe na moto iwe makaa, kama vile wengine wanavyoamini, wala iharibiwe na makombora ya nyukilia, kama vile wengine wanavyohofu. Mungu anakusudia dunia ibaki milele, ikiwa imepambwa uzuri wa kiparadiso na kukaliwa na wakaaji wenye haki. (Zaburi 37:11, 29; 115:16; Mathayo 6:9, 10; Ufunuo 21:3, 4) Ndiyo, maneno ya Yehova yatategemeka kama vile yalivyotegemeka kuhusu Israeli.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki