-
Kuirudia Ibada ya YehovaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Mjipe Moyo”
11. Ni nini kitakachowasaidia wale wanaoyumbayumba ‘wajipe moyo’?
11 Baada ya kuonyesha ubatili wa kuabudu sanamu, sasa Yehova anawapa watu wake sababu ambazo inawapasa wamtumikie yeye: “Kumbukeni haya, mkajionyeshe kuwa waume [“mjipe moyo,” “NW”]; jifahamisheni haya, ninyi mkosao;
-
-
Kuirudia Ibada ya YehovaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Wale wanaoyumbayumba kati ya ibada ya kweli na ibada ya sanamu wanapaswa waikumbuke historia. Wanapaswa kuzingatia mambo ambayo Yehova amefanya. Hiyo itawasaidia wajipe moyo kutenda lililo haki. Itawasaidia warudie kumwabudu Yehova.
12, 13. Wakristo wamekabwa katika mapambano gani, na wanaweza kushinda jinsi gani?
12 Kitia-moyo hicho kingali kinahitajiwa leo. Hali moja na Waisraeli, Wakristo wanyofu hulazimika kupigana na vishawishi na hali zao wenyewe za kutokamilika. (Waroma 7:21-24) Isitoshe, wamekabana na adui asiyeonekana mwenye nguvu sana katika vita vya kiroho. Mtume Paulo anasema hivi: “Tuna kushindana mwereka, si dhidi ya damu na mwili, bali dhidi ya serikali, dhidi ya mamlaka, dhidi ya watawala wa ulimwengu wa giza hili, dhidi ya majeshi ya roho waovu katika mahali pa kimbingu.”—Waefeso 6:12.
13 Shetani na roho wake waovu watajitahidi kufa na kupona kujaribu kuwaondoa Wakristo katika ibada ya kweli. Ili Wakristo wafanikishe pigano lao, wanahitaji kufuata shauri la Yehova na kujipa moyo. Jinsi gani? Mtume Paulo anaeleza hivi: “Vaeni suti kamili ya silaha kutoka kwa Mungu ili mpate kuweza kusimama imara dhidi ya mbinu za Ibilisi.” Yehova hawapeleki watumishi wake piganoni wakiwa na vifaa ovyo. Silaha zao za kiroho zinahusisha ‘ngao kubwa ya imani, ambayo kwayo wataweza kuzima vishale vyote vinavyowaka moto vya yule mwovu.’ (Waefeso 6:11, 16) Waisraeli walikuwa wakosaji kwa sababu waliyapuuza maandalizi ya kiroho ambayo Yehova alikuwa amewafanyia. Kama wangaliyafikiria maajabu ambayo Yehova aliwafanyia tena na tena, wasingaligeuka kamwe kuziabudu sanamu zenye kuchukiza. Na tujifunze kutokana na mfano wao, tupige moyo konde kwamba hatutayumbayumba kamwe katika pigano la kutenda haki.—1 Wakorintho 10:11.
-