Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Babiloni Yashushwa Chini Kwenye Vumbi

      3. Fafanua ukuu wa Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Babiloni.

      3 Ebu lisikilize tangazo hili rasmi la kimungu linalosisimua: “Haya, shuka, keti mavumbini, ewe bikira, binti Babeli; keti chini pasipo kiti cha enzi, ewe binti wa Wakaldayo; maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.” (Isaya 47:1) Kwa miaka mingi, Babiloni amekalia kiti cha ufalme akiwa serikali kubwa ya ulimwengu yenye mamlaka. Amekuwa “utukufu wa falme”—kitovu chenye usitawi wa kidini, wa kibiashara na wa kijeshi. (Isaya 13:19) Babiloni anapofikia upeo, milki yake imetandaa hadi mbali kusini kwenye mpaka wa Misri. Kisha, anapomshinda Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K., inaonekana ni kama Mungu mwenyewe hawezi kumzuia kupata-pata ushindi! Basi, Babiloni anajiona kuwa ‘binti bikira,’ ambaye hataingiliwa kamwe na mvamizi wa kigeni.b

      4. Babiloni atapatwa na nini?

      4 Hata hivyo, “bikira” huyo kichwa kikubwa atadondoshwa kutoka kwenye kiti chake cha kifalme asiwe tena serikali kubwa ya ulimwengu isiyoweza kubishaniwa, ‘aketishwe mavumbini’ kwa kutiwa aibu. (Isaya 26:5) Hataonwa tena kuwa “mwororo, mpenda anasa,” mfano wa malkia wa kubembelezwa-bembelezwa.

  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • b Kwa Kiebrania, “bikira, binti Babeli” ni msemo unaomaanisha Babiloni au wakaaji wa Babiloni. Yeye ni “bikira” kwa sababu hakuna mshindi amewahi kumteka nyara tangu awe serikali kubwa ya ulimwengu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki