Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 9. Kwa nini Yehova anawakasirikia Wayahudi kwa haki?

      9 Kwanza hata imekuwaje Babiloni akaruhusiwa kuwadhuru watu wa Mungu? Yehova anaeleza hivi: “Nalikuwa nimekasirika na watu wangu, naliutia unajisi urithi wangu, nikawatia mkononi mwako.” (Isaya 47:6a) Yehova ana sababu nzuri ya kuwakasirikia Wayahudi. Zamani zile, aliwaonya kwamba wasipoitii Sheria yake wangefukuzwa nchini. (Kumbukumbu la Torati 28:64) Walipotumbukia katika ibada ya sanamu na ukosefu wa adili kingono, Yehova alionyesha upendo kwa kutuma manabii wakawasaidie kuirudia ibada safi. “Lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya BWANA juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.” (2 Mambo ya Nyakati 36:16) Basi, wakati Babiloni anapovamia Yuda na kuchafua hekalu Lake takatifu, Mungu anaruhusu nchi hiyo, iliyo urithi wake, itiwe unajisi.—Zaburi 79:1; Ezekieli 24:21.

      10, 11. Kwa nini Yehova anakasirikia Babiloni, hata ingawa ni mapenzi yake kwamba Babiloni awashinde watu wake?

      10 Basi, je, Babiloni anapowatumikisha Wayahudi, hafanyi hivyo ili kutimiza mapenzi ya Mungu tu? Sivyo, kwani Mungu anasema hivi: “Wewe hukuwatendea rehema; uliwatia wazee nira yako, nayo nzito sana.

  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Isaya 47:6b,

  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Mungu hajampa Babiloni amri ya kuwa mkatili mno, hivi kwamba hata hawawaonyeshi “wazee” hisani. (Maombolezo 4:16; 5:12) Wala hajawahimiza wajifurahishe kinyama kwa kuwadhihaki mateka Wayahudi.—Zaburi 137:3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki