-
Yehova Hutufundisha kwa Faida YetuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
3. Ibada ya Yuda ilikuwa na kasoro gani?
3 Lo, watu wa Yehova wamekengeuka mbali kama nini kutoka kwenye ibada safi! Maneno ya utangulizi ya Isaya yanahitaji kufikiriwa kwa makini: “Sikieni haya, enyi watu wa nyumba ya Yakobo, mnaoitwa kwa jina la Israeli, mliotoka katika maji ya Yuda; mnaoapa kwa jina la BWANA [“Yehova,” “NW”], na kumtaja Mungu wa Israeli, lakini si kwa kweli, wala si kwa haki.
-
-
Yehova Hutufundisha kwa Faida YetuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Unafiki kama nini! Ni wazi kwamba ‘kuapa kwa jina la Yehova’ ni kutumia jina la Mungu kidesturi tu. (Sefania 1:5) Kabla ya kuhamishiwa Babiloni, Wayahudi walimwabudu Yehova kwenye “mji mtakatifu,” Yerusalemu. Lakini ibada yao haikuwa ya moyo mweupe. Mioyo yao ilikuwa mbali sana na Mungu, na vitendo vyao vya ibada vilikuwa ‘si vya kweli, wala si vya haki.’ Hawakuwa na imani kama ile ya wazee wa ukoo.—Malaki 3:7.
4. Ni ibada ya aina gani inayompendeza Yehova?
4 Maneno ya Yehova yanatukumbusha kwamba ibada haipaswi kuwa desturi ya kijuujuu tu. Ni lazima ifanywe kwa hisia za moyoni. Utumishi wa kuonyesha tu—labda unaofanywa ili kuwafurahisha au kuwavutia wengine tu—si “vitendo vya ujitoaji-kimungu.” (2 Petro 3:11) Ibada ya mtu haikubaliki kwa Mungu eti kwa sababu tu mtu anajiita Mkristo. (2 Timotheo 3:5) Ni muhimu kutambua kwamba Yehova yuko, lakini huo ni mwanzo tu. Yehova anataka ibada ya nafsi yote, inayoongozwa na upendo wa kina kirefu na uthamini.—Wakolosai 3:23.
-