-
Yehova Hutufundisha kwa Faida YetuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Je, yale ambayo Yehova anasema sasa yataleta angalau badiliko fulani juu ya Wayahudi wasio waaminifu? Mungu anawaambia hivi: “Umesikia haya; tazama haya yote; nanyi, je! hamtayahubiri? Nimekuonyesha mambo mapya tangu wakati huu, naam, mambo yaliyofichwa, usiyoyajua.
-
-
Yehova Hutufundisha kwa Faida YetuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
7. Wayahudi wahamishwa watalazimika kukiri nini, na wanaweza kutazamia nini?
7 Isaya aliandika utabiri wa anguko la Babiloni kitambo kirefu kabla halijatukia. Sasa Wayahudi wakiwa wahamishwa Babiloni, wanaamrishwa kiunabii wafikirie sana utimizo wa utabiri huo. Je, sasa wanaweza kukana kwamba Yehova siye Mungu wa unabii uliotimizwa? Na kwa kuwa wakaaji wa Yuda wameona na kusikia kwamba Yehova ni Mungu wa kweli, je, hawana budi kuwatangazia wengine pia kweli hiyo? Neno la Yehova lililofunuliwa linatabiri mapya ambayo bado hayajatokea, kwa mfano ushindi wa Koreshi juu ya Babiloni na kufunguliwa kwa Wayahudi. (Isaya 48:14-16)
-
-
Yehova Hutufundisha kwa Faida YetuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Unabii mbalimbali uliotimizwa unathibitisha Uungu wake kwa Wayahudi wa nyakati za kale na hali kadhalika kwa Wakristo wa leo. Maandishi yaliyopo kuhusu unabii mwingi sana uliotimizwa wakati uliopita, ambao ndio “mambo ya kale,” yanahakikisha kwamba yale mambo mapya yaliyoahidiwa na Yehova, yaani “dhiki kubwa” inayokuja, kuokoka kwa “umati mkubwa” kwa kuipita dhiki hiyo, “dunia mpya,” na mengine kadha wa kadha, yatatimizwa pia. (Ufunuo 7:9, 14, 15; 21:4, 5; 2 Petro 3:13) Uhakikisho huo huwasukuma wale walio na mioyo ya kupenda haki leo wanene habari zake kwa bidii. Wao wanajihisi kama mtunga-zaburi, aliyesema hivi: “Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa. Sikuizuia midomo yangu.”—Zaburi 40:9.
-