-
Yehova Hutufundisha kwa Faida YetuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
16, 17. (a) Kwa nini inaweza kusemwa kwamba Mungu hajatoa matabiri yake kwa siri? (b) Leo Yehova ameyajulishaje makusudi yake peupe?
16 Yehova anaendelea kusema hivi kwa sauti nzuri ya mwaliko: “Nikaribieni, sikieni haya; tokea mwanzo sikunena kwa siri; tangu yalipokuwapo, mimi nipo.” (Isaya 48:16a) Matabiri kutoka kwa Yehova hayajatolewa kwa siri wala kujulishwa kwa washiriki wachache tu wa kikundi maalumu. Manabii wa Yehova walikuwa wasemaji waliosema mambo waziwazi kwa niaba ya Mungu. (Isaya 61:1) Walitangaza mapenzi ya Mungu peupe. Kwa mfano, matukio yaliyomhusu Koreshi hayakuwa mapya kwa Mungu wala hayakutukia bila yeye kuyaona kimbele. Miaka 200 hivi mapema, Mungu aliyatabiri matukio hayo waziwazi kupitia Isaya.
17 Vivyo hivyo leo, Yehova haweki makusudi yake kuwa siri. Mamilioni ya watu katika mamia ya nchi na visiwa vya bahari hutangaza nyumba kwa nyumba, barabarani, na popote pale wawezapo juu ya onyo linalohusu mwisho unaokuja wa mfumo huu wa mambo, na pia juu ya habari njema za baraka zitakazokuja chini ya Ufalme wa Mungu. Kweli Yehova ni Mungu wa mawasiliano kuhusu makusudi yake.
‘Sikiliza Amri Zangu!’
18. Yehova anatamani nini kuhusu watu wake?
18 Akiwa ametiwa nguvu na roho ya Yehova, nabii anatangaza rasmi hivi: “Bwana MUNGU amenituma, na roho yake.
-