Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Hutufundisha kwa Faida Yetu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • BWANA, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.” (Isaya 48:16b, 17) Wonyesho huu wenye upendo wa kujali kwa Yehova unapasa kulihakikishia upya taifa la Israeli kwamba Mungu atawakomboa kutoka Babiloni. Yeye ndiye Mkombozi wao. (Isaya 54:5) Yehova anatamani kwa hisia za moyoni kwamba Waisraeli warudishe uhusiano wao naye na kuzisikiliza amri zake. Kutii maagizo ya kimungu ndio msingi wa ibada ya kweli. Waisraeli hawawezi kutembea katika njia ifaayo wasipofundishwa ‘njia iwapasayo kuifuata.’

  • Yehova Hutufundisha kwa Faida Yetu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 21. Ni baraka gani tunazoweza kuzipata leo tukiyatafuta mafundisho ya Yehova?

      21 Kanuni zilizomo katika kifungu hicho chenye mkazo zinatumika kuwahusu waabudu wa Yehova leo. Yehova ndiye Chanzo cha uhai, na ndiye anayejua zaidi ya mtu mwingine yeyote jinsi itupasavyo kutumia maisha yetu. (Zaburi 36:9) Lengo la miongozo ambayo ametupa si kutunyang’anya furaha, bali ni kutunufaisha. Wakristo wa kweli huitikia kwa kutafuta kufundishwa na Yehova. (Mika 4:2) Maelekezo yake huilinda hali yetu ya kiroho na uhusiano wetu pamoja naye, tena hutukinga na mavutano ya Shetani yenye kufisidi. Tunapozithamini kanuni zilizo msingi wa sheria za Mungu, tunaona kwamba Yehova hutufundisha kwa faida yetu. Tunatambua kwamba “amri zake si zenye kulemea.” Na hatutakatiliwa mbali.—1 Yohana 2:17; 5:3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki