Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakati wa Nia Njema”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 8. Watu wa Mesiya mwenyewe wanamwitikiaje, lakini Mesiya anategemea nani kuhukumu mafanikio yake?

      8 Lakini je, si kweli kwamba Yesu anadharauliwa na kukataliwa na wengi wa watu wake mwenyewe? Ndiyo. Kwa ujumla, taifa la Israeli halimkubali Yesu kuwa Mtumishi mtiwa-mafuta wa Mungu. (Yohana 1:11) Huenda marika wa Yesu wakayaona yote anayoyatimiza akiwa duniani kama yasiyo na thamani kubwa, hata yasiyofaa kitu. Ndipo sasa Mesiya anapogusia hali hiyo ya kuonekana kana kwamba ameshindwa kuitimiza huduma yake: “Nimejitaabisha bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida.” (Isaya 49:4a) Maneno hayo hayasemwi eti kwa sababu Mesiya amevunjika moyo. Yafikirie yale anayosema sasa: “Hakika hukumu yangu ina BWANA, na thawabu yangu ina [“mshahara wangu una,” “NW”] Mungu wangu.” (Isaya 49:4b) Mafanikio ya Mesiya hayaamuliwi na wanadamu, bali na Mungu.

  • “Wakati wa Nia Njema”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 10 Leo, nyakati fulani huenda wafuasi wa Yesu wakahisi kana kwamba wanatoa jasho la bure. Mahali fulani fulani, huenda matokeo ya huduma yao yakaonekana kuwa si kitu yakilinganishwa na kiasi cha kazi na jitihada wanazofanya. Hata hivyo, wao huvumilia kwa kutiwa moyo na mfano wa Yesu. Wanatiwa nguvu pia na maneno ya mtume Paulo, aliyeandika hivi: “Kwa sababu hiyo, ndugu zangu wapendwa, iweni imara, wasioondoleka, sikuzote mkiwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi yenu ya jasho si bure kuhusiana na Bwana.”—1 Wakorintho 15:58.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki