Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakati wa Nia Njema”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 15. Ni “wakati” gani maalumu unaotajwa katika unabii wa Isaya, na hiyo inatoa wazo gani?

      15 Unabii wa Isaya unaendelea kwa kutoa taarifa yenye umaana mkubwa. Yehova anamwambia Mesiya hivi: “Wakati uliokubalika [“wakati wa nia njema,” “NW”] nimekujibu, na siku ya wokovu nimekusaidia; nami nitakuhifadhi, nitakutoa uwe agano la watu hawa.” (Isaya 49:8a) Unabii unaofanana na huo umeandikwa kwenye Zaburi 69:13-18. Mtunga-zaburi anarejezea “wakati wa nia njema,” akitumia usemi ‘wakati upendezao.’ Maneno haya yanatokeza wazo la kwamba nia njema ya Yehova na ulinzi wake hutolewa kwa njia maalumu lakini kwa kipindi hususa cha muda mfupi tu.

      16. Wakati wa Yehova wa nia njema kwa Israeli wa kale ulikuwa lini?

      16 Wakati huo wa nia njema ulikuwa lini? Maneno hayo yaliposemwa mara ya kwanza yalikuwa sehemu ya unabii wa kurudishwa na yalitabiri kurudi kwa Wayahudi kutoka uhamishoni. Taifa la Israeli lilipata wakati wa nia njema lilipoweza “kuiinua nchi” na kumiliki tena “urithi uliokuwa ukiwa.” (Isaya 49:8b)

  • “Wakati wa Nia Njema”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Ijapokuwa utimizo huo wa kwanza wa kutazamisha ulitukia, Biblia inaonyesha kwamba unabii huu unatumika kwa njia nyinginezo zilizo pana.

      17, 18. Yehova aliweka wakati gani wa nia njema katika karne ya kwanza?

      17 Kwanza, wakati wa kuzaliwa kwa Yesu, malaika walitangaza amani na nia njema ya Mungu, au upendeleo wake, kuelekea wanadamu. (Luka 2:13, 14) Nia njema hiyo ilitolewa iweze kupatikana, si na wanadamu wote kwa ujumla, bali na wale tu waliodhihirisha imani katika Yesu. Baadaye Yesu aliusoma peupe unabii wa Isaya 61:1, 2 na kuutumia umhusu yeye mwenyewe akiwa mtangazaji wa “mwaka wa Yehova wenye kukubalika.” (Luka 4:17-21) Mtume Paulo alitaja kwamba Kristo alipokea ulinzi maalumu wa Yehova katika siku za mwili wake. (Waebrania 5:7-9) Kwa hiyo wakati huu wa nia njema unatumika kuhusu upendeleo ambao Mungu alimwonyesha Yesu wakati wa maisha yake akiwa binadamu.

      18 Hata hivyo, unabii huu una matumizi zaidi. Baada ya kuyanukuu maneno ya Isaya kuhusu wakati wa nia njema, Paulo aliendelea kusema hivi: “Tazameni! Sasa ndio wakati wenye kukubalika hasa. Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” (2 Wakorintho 6:2) Paulo aliyaandika maneno haya miaka 22 baada ya kifo cha Yesu. Ushuhuda unaonyesha kuwa kutaniko la Kikristo lilipozaliwa Pentekoste ya 33 W.K., Yehova aliurefusha mwaka wake wa nia njema ili uwahusishe pia wafuasi watiwa-mafuta wa Kristo.

      19. Wakristo leo wanaweza kunufaikaje na wakati wa Yehova wa nia njema?

      19 Namna gani wafuasi wa Yesu leo wasiotiwa mafuta kuwa warithi wa ufalme wa kimbingu wa Mungu? Je, wale walio na tumaini la kidunia wanaweza kunufaika na wakati huu uliokubalika? Ndiyo. Kitabu cha Biblia cha Ufunuo kinaonyesha kwamba huu ni wakati wa nia njema kwa upande wa Yehova kuelekea umati mkubwa ‘utakaotoka katika dhiki kubwa’ ili kufurahia maisha katika dunia-paradiso. (Ufunuo 7:13-17) Kwa hiyo, Wakristo wote wana fursa ya kukitumia vizuri kipindi hiki kifupi ambacho Yehova huwatolea nia yake njema wanadamu wasio wakamilifu.

      20. Wakristo wanaweza kuepukaje kulikosa kusudi la fadhili isiyostahiliwa ya Yehova?

      20 Mtume Paulo alitoa onyo kabla ya kuutangaza wakati wa Yehova unaokubalika. Aliwasihi Wakristo ‘wasiipokee fadhili isiyostahiliwa ya Mungu na kukosa kusudi lake.’ (2 Wakorintho 6:1) Kwa hiyo, Wakristo hutumia kila fursa wampendeze Mungu na kufanya mapenzi yake. (Waefeso 5:15, 16) Inafaa wafuate onyo la upole la Paulo: “Jihadharini, akina ndugu, kwa kuhofu kusije kamwe kukasitawi katika yeyote kati yenu moyo mwovu unaokosa imani kwa kujiondoa kwa Mungu aliye hai; lakini fulizeni kuhimizana kwa bidii mtu na mwenzake kila siku, maadamu yaweza kuitwa ‘Leo,’ kwa kuhofu yeyote kati yenu asije akafanywa kuwa mgumu kwa nguvu ya udanganyifu ya dhambi.”—Waebrania 3:12, 13.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki