-
“Wakati wa Nia Njema”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Akitenda kama msemaji wa Yehova, Isaya anaendelea kusema hivi: “Je! mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.” (Isaya 49:15) Hilo ni itikio lenye upendo kama nini kutoka kwa Yehova! Upendo wa Mungu kwa watu wake ni mkubwa kuliko ule wa mama kwa mtoto wake.
-
-
“Wakati wa Nia Njema”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
23. Paulo aliwatiaje moyo Wakristo watumainie kuwa Yehova hatawasahau?
23 Katika barua yake kwa Wagalatia, mtume Paulo aliwahimiza Wakristo hivi: “Acheni tusife moyo katika kufanya lililo bora, kwa maana katika majira yapasayo tutavuna ikiwa hatuchoki kabisa.” (Wagalatia 6:9) Aliwaandikia Waebrania maneno haya ya kuwatia moyo: “Mungu si asiye mwadilifu ili asahau kazi yenu na upendo mlioonyesha kwa ajili ya jina lake.” (Waebrania 6:10) Hatupaswi kamwe kuhisi kwamba Yehova amewasahau watu wake. Kama Sayuni wa kale, Wakristo wana sababu nzuri ya kushangilia na kumngoja Yehova kwa subira. Yeye huyashika imara masharti ya agano lake na ahadi zake.
-