Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Msiwatumainie Wakuu”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 17. Yehova amemtegemeza Yesu kwa njia zipi muda wote wa huduma yake?

      17 Yesu anafaulu kuwa na moyo mkuu kwa sababu anamtumaini Yehova kabisa. Jinsi anavyojichukua inaonyesha kwamba anayafuata maneno haya ya Isaya kwa ukamili: “Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu; ni nani atakayeshindana nami? Na tusimame pamoja; ni nani aliye hasimu yangu? Na anikaribie basi.

  • “Msiwatumainie Wakuu”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Isaya 50:8,

  • “Msiwatumainie Wakuu”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Siku ya ubatizo wa Yesu, Yehova anamtangaza kuwa mwenye haki akiwa mwana wa kiroho wa Mungu. Kwa kweli, sauti ya Mungu mwenyewe inasikiwa pindi hiyo ikisema hivi: “Huyu ni Mwana wangu, mpendwa, ambaye nimemkubali.” (Mathayo 3:17) Maisha ya Yesu ya kidunia yanapokaribia kumalizika, anaposali akiwa amepiga magoti katika bustani ya Gethsemane, ‘malaika kutoka mbinguni anamtokea na kumtia nguvu.’ (Luka 22:41-43) Kwa hiyo Yesu anajua kwamba Baba yake anaukubali mwendo wa maisha yake. Mwana huyu mkamilifu wa Mungu hajatenda dhambi. (1 Petro 2:22) Adui zake wanamshtaki kwa uwongo kuwa mvunja-Sabato, mlevi, na mtu mwenye roho waovu, lakini Yesu havunjiwi heshima na mashtaka yao ya uwongo. Mungu yuko pamoja naye, basi ni nani awezaye kumpinga?—Luka 7:34; Yohana 5:18; 7:20; Waroma 8:31; Waebrania 12:3.

      18, 19. Wakristo watiwa-mafuta wamepatwa na mambo gani yaliyompata Yesu pia?

      18 Yesu anawaonya wanafunzi wake hivi: “Ikiwa wameninyanyasa mimi, watawanyanyasa nyinyi pia.” (Yohana 15:20) Muda si muda, mambo yanayotukia yanathibitisha ukweli wa maneno hayo. Kwenye Pentekoste ya 33 W.K., roho takatifu inawajilia wanafunzi waaminifu wa Yesu, na hapo kutaniko la Kikristo linazaliwa. Haujapita muda, viongozi wa kidini wanajaribu kuikandamiza kazi ya kuhubiri ya wanaume na wanawake hao waaminifu ambao sasa wanashirikiana na Yesu wakiwa sehemu ya “mbegu ya Abrahamu” na kufanywa wana wa kiroho wa Mungu. (Wagalatia 3:26, 29; 4:5, 6) Ingawa Wakristo watiwa-mafuta wanasimama imara upande wa uadilifu, tangu karne ya kwanza mpaka sasa wamelazimika kushindana na propaganda za uwongo na mnyanyaso mkatili sana kutoka kwa adui za Yesu.

      19 Na bado wanayakumbuka maneno ya Yesu yenye kutia moyo: “Wenye furaha ni nyinyi watu wawashutumupo na kuwanyanyasa nyinyi na kusema kwa uwongo kila namna ya jambo ovu dhidi yenu kwa ajili yangu. Shangilieni na kuruka kwa shangwe, kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa katika mbingu.” (Mathayo 5:11, 12) Hivyo basi, Wakristo watiwa-mafuta wanaona fahari hata chini ya shambulio kali kupita yote. Hata wapinzani wao wasemeje, Mungu amekwisha kuwatangaza rasmi kuwa waadilifu. Machoni pake, wao ‘hawana waa na lawama yoyote.’—Wakolosai 1:21, 22.

      20. (a) Ni akina nani wanaowaunga mkono Wakristo watiwa-mafuta, nao wamejionea nini? (b) Ni jinsi gani Wakristo watiwa-mafuta na “kondoo wengine” wanavyokuja kuwa na ulimi wa wale waliofundishwa?

      20 Nyakati za kisasa, Wakristo watiwa-mafuta wanaungwa mkono na “umati mkubwa” wa “kondoo wengine.” Wao pia wanasimama upande wa uadilifu. Kwa hiyo, wameteseka pamoja na ndugu zao watiwa-mafuta na “wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Yehova amewatangaza rasmi kuwa waadilifu wakiwa na tazamio la kuiokoka “dhiki kubwa.” (Ufunuo 7:9, 14, 15; Yohana 10:16; Yakobo 2:23)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki