-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
2. Sayuni anaamka lini, na hilo linatukiaje?
2 Yehova anamtumia Isaya kupaza sauti akitoa mwito ufuatao kwa Sayuni, jiji Lake kipenzi: “Amka, amka, jivike nguvu zako, Ee Sayuni; jivike mavazi yako mazuri, Ee Yerusalemu, mji mtakatifu; kwa maana tokea sasa hataingia ndani yako asiyetahiriwa, wala aliye najisi.
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Yerusalemu amelala ukiwa muda wa miaka 70 kwa sababu wakaaji wake wameichochea hasira ya Yehova. (2 Wafalme 24:4; 2 Mambo ya Nyakati 36:15-21; Yeremia 25:8-11; Danieli 9:2) Sasa wakati umefika aamke kutoka kwenye kipindi chake kirefu cha kutokutenda, ajivike mavazi mazuri ya ukombozi. Yehova ameugusa moyo wa Koreshi kumweka huru ‘binti Sayuni aliyefungwa’ ili wakaaji wa zamani wa Yerusalemu na wazao wao waweze kuondoka Babiloni, warudi Yerusalemu, warudishe ibada ya kweli. Watu wowote wasiotahiriwa na walio najisi hawapaswi kamwe kuwako Yerusalemu.—Ezra 1:1-4.
3. Kwa nini kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta linaweza kuitwa “binti Sayuni,” nao wanakombolewa katika maana gani?
3 Maneno hayo ya Isaya yana utimizo unaohusu kutaniko la Kikristo pia. Kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta linaweza kufafanuliwa kuwa “binti Sayuni” wa kisasa, kwa kuwa “Yerusalemu la juu” ndiye mama yao.a Kwa kuwa watiwa-mafuta wamewekwa huru kutokana na mafundisho ya kipagani na ya uasi-imani, ni lazima wadumishe msimamo safi mbele za Yehova, si kwa kutahiriwa mwili, hapana, bali kwa kutahiriwa katika mioyo yao. (Yeremia 31:33; Waroma 2:25-29) Hiyo inahusisha kudumisha usafi wa kiroho, wa kiakili, na wa kiadili mbele za Yehova.—1 Wakorintho 7:19; Waefeso 2:3.
4. Ingawa “Yerusalemu la juu” halijakosa kamwe kumtii Yehova, ni mambo gani yaliyowapata wawakilishi wake duniani yanayofanana na yale ya wakaaji wa kale wa Yerusalemu?
4 Ni kweli kwamba “Yerusalemu la juu” halijakosa kamwe kumtii Yehova. Hata hivyo, wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, wawakilishi wake duniani—Wakristo watiwa-mafuta—walivunja sheria ya Yehova bila kujua kwa sababu hawakuuelewa vizuri msimamo wa kweli wa kutokuwamo kwa Kikristo. Walipoteza upendeleo wa kimungu, wakaingia katika utekwa wa kiroho wa “Babiloni Mkubwa,” ile milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo. (Ufunuo 17:5) Upeo wa utumwa wao ulifika Juni 1918 wakati washirika wanane kati ya wafanyakazi wa Watch Tower Society walipofungwa gerezani kwa mashtaka ya uwongo, mojawapo likiwa ni kufanya uhaini. Hapo basi kazi ya kuhubiri habari njema kwa mpangilio mzuri ikawa ni kama imekoma. Lakini, mwaka wa 1919 mbiu ikapigwa kuwaita waamke kiroho. Wakristo watiwa-mafuta walianza kujitenga kwa ukamili zaidi na uchafu wa kiadili na wa kiroho wa Babiloni Mkubwa. Waliinuka kutoka kwenye mavumbi ya utekwa, nalo “Yerusalemu la juu” likapata fahari ya kuwa “mji mtakatifu” ambapo uchafu wa kiroho hauruhusiwi.
-