-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
7. Utekwa wa watu wa Yehova umekuwa na matokeo gani juu ya jina lake?
7 Utekwa wa watu wa Yehova unaathiri jina lake, kama vile unabii unavyoonyesha: “Basi sasa, nafanya nini hapa [“ninapata faida gani hapa,” “NW”], asema BWANA, ikiwa watu wangu wamechukuliwa bure? Hao wanaowatawala wanapiga yowe, asema BWANA, na jina langu linatukanwa daima mchana kutwa.
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Yehova anapata faida gani katika hali hiyo? Mbona ahangaike kwamba Israeli wamewekwa utumwani Babiloni? Ni lazima Yehova achukue hatua kwa sababu Babiloni amewateka watu wake na kuwapigia yowe la shangwe ya ushindi. Kujigamba huko kumefanya Babiloni alidharau jina la Yehova. (Ezekieli 36:20, 21) Babiloni ameshindwa kutambua kwamba Yerusalemu limekuwa ukiwa kwa sababu Yehova amechukizwa na watu wake. Badala yake, Babiloni ameuona utumwa wa Wayahudi kuwa ni ushahidi wa kuonyesha kwamba Mungu wao ni dhaifu. Belshaza, mtawala-msaidizi wa Babiloni, hata anamdhihaki Yehova kwa kutumia vyombo kutoka kwenye hekalu Lake wakati wa karamu ya kuheshimu miungu ya Babiloni.—Danieli 5:1-4.
8. Jina la Yehova limetendewaje tangu mitume walipokufa?
8 Hayo yote yanahusuje “Yerusalemu la juu”? Tangu uasi-imani utie mizizi miongoni mwa wale wanaojiita Wakristo, ingeweza kusemwa kwamba “jina la Mungu linafanyiwa kufuru miongoni mwa mataifa kwa sababu ya [hao] watu.” (Waroma 2:24; Matendo 20:29, 30) Hivyo basi, hatimaye Wayahudi walianza kuepuka kutumia jina la Mungu kwa hofu ya kishirikina. Upesi baada ya kifo cha mitume, Wakristo waasi-imani walifuata mkondo huo huo wakaacha kulitumia jina la kibinafsi la Mungu. Jumuiya ya Wakristo, ambayo ni sehemu kubwa ya Babiloni Mkubwa, ilisitawi kutokana na uasi-imani huo. (2 Wathesalonike 2:3, 7; Ufunuo 17:5) Jina la Yehova limepata sifa mbaya kwa sababu ya ukosefu wa adili ulioenea sana katika Jumuiya ya Wakristo na hatia yake ya kumwaga damu kwa macho makavu.—2 Petro 2:1, 2.
-