Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 21. (a) Wale ‘wanaochukua vyombo vya Yehova’ wanatakiwa wafanye nini? (b) Kwa nini Wayahudi wanaoondoka Babiloni hawana sababu ya kubabaika kwa hofu?

      21 Wale wanaotoka Babiloni kurudi Yerusalemu wana takwa fulani la kutimiza. Isaya anaandika hivi: “Nendeni zenu, nendeni zenu, tokeni huko, msiguse kitu kichafu; tokeni kati yake; iweni safi ninyi mnaochukua vyombo vya BWANA.

  • ‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Isaya 52:11,

  • ‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Ni lazima Waisraeli wanaoondoka waache huko Babiloni kitu chochote kilicho na doa la ibada ya uwongo ya Babiloni. Kwa kuwa wanachukua vyombo vya Yehova vilivyotoka hekaluni Yerusalemu, ni lazima wawe safi moyoni hasa, wala si kwa nje tu, kwa kufuata desturi fulani rasmi. (2 Wafalme 24:11-13; Ezra 1:7)

  • ‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 22. Paulo anakaziaje uhitaji wa usafi miongoni mwa Wakristo watiwa-mafuta?

      22 Maneno ya Isaya kuhusu kuendelea kuwa safi yanatimizwa kwa kadiri kubwa juu ya wazao wa “Yerusalemu la juu.” Paulo alipowaonya kwa upole Wakristo Wakorintho wasifungwe nira pamoja na wasio waamini kwa njia isiyosawazika, aliyanukuu maneno ya Isaya 52:11: “‘Kwa hiyo tokeni miongoni mwao, na jitengeni wenyewe,’ asema Yehova, ‘na komeni kugusa kitu kisicho safi.’” (2 Wakorintho 6:14-17) Sawa na vile ilivyokuwa kwa Waisraeli wakielekea nyumbani kutoka Babiloni, ni lazima Wakristo waepuke kabisa ibada ya uwongo ya Kibabiloni.

      23. Watumishi wa Yehova leo hujitahidi kujidumisha wakiwa safi kwa njia zipi?

      23 Ndivyo hasa ilivyokuwa kwa habari ya wale wafuasi watiwa-mafuta wa Yesu Kristo waliokimbia kutoka Babiloni Mkubwa mwaka wa 1919. Walijisafisha hatua kwa hatua wakajiondolea dalili zote zilizobaki za ibada ya uwongo. (Isaya 8:19, 20; Waroma 15:4) Pia walipata ufahamu zaidi kuhusu umuhimu wa usafi wa kiadili. Ingawa nyakati zote Mashahidi wa Yehova wametetea viwango vya juu vya kiadili, mwaka wa 1952 gazeti Mnara wa Mlinzi lilikuwa na makala zilizokazia uhitaji wa kuwatia nidhamu wakosefu wa adili ili kudumisha usafi wa kutaniko. Hatua hiyo ya nidhamu humsaidia mkosaji mwenyewe atambue uhitaji wa kutubu kwa moyo mweupe.—1 Wakorintho 5:6, 7, 9-13; 2 Wakorintho 7:8-10; 2 Yohana 10, 11.

      24. (a) ‘Vyombo vya Yehova’ ni nini nyakati za kisasa? (b) Kwa nini Wakristo leo wana uhakika kwamba Yehova ataendelea kutangulia mbele yao na pia awe mlinzi nyuma yao?

      24 Wakristo watiwa-mafuta pamoja na ule umati mkubwa wa kondoo wengine wamepiga moyo konde kutogusa kitu chochote chenye uchafu wa kiroho. Hali yao iliyotiwa utakato na usafi huwastahilisha wawe wachukuaji wa ‘vyombo vya Yehova.’ Vyombo hivyo ni yale maandalizi ya thamani kubwa ambayo Mungu hufanya ili yatumiwe katika utumishi mtakatifu wa huduma ya nyumba kwa nyumba na ya funzo la Biblia na namna nyingine za utendaji wa Kikristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki