-
Yehova Amkweza Mtumishi Wake wa KimesiyaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
‘Alijiacha Aumizwe’
25. Tunajuaje kwamba Mesiya aliteseka na kufa kwa hiari?
25 Je, Mesiya alikuwa na hiari ya kuteseka na kufa? Isaya anasema hivi: “Alionewa, lakini alinyenyekea [“alikuwa akijiacha aumizwe,” “NW”], wala hakufunua kinywa chake; kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, na kama vile kondoo anyamazavyo mbele yao wakatao manyoya yake; naam, hakufunua kinywa chake.” (Isaya 53:7) Katika usiku wa mwisho wa maisha yake, Yesu angaliweza kuagiza “malejioni zaidi ya kumi na mawili ya malaika” yaje kumsaidia. Lakini yeye alisema hivi: “Katika kisa hicho, Maandiko yangetimizwaje kwamba lazima itendeke kwa njia hii?” (Mathayo 26:53, 54) “Mwana-Kondoo wa Mungu” hakutokeza upinzani wowote. (Yohana 1:29) Makuhani wakuu na wanaume wazee walipomshtaki kwa uwongo mbele ya Pilato, Yesu “hakutoa jibu.” (Mathayo 27:11-14) Hakutaka kusema lolote ambalo lingaliweza kumvuruga asitimize mapenzi ya Mungu kumhusu. Yesu alikuwa na hiari ya kufa akiwa Mwana-Kondoo wa dhabihu, akijua vema kabisa kwamba kifo chake kingekomboa wanadamu watiifu kutoka kwenye dhambi, ugonjwa, na kifo.
-
-
Yehova Amkweza Mtumishi Wake wa KimesiyaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
[Picha katika ukurasa wa 206]
“Hakufunua kinywa chake”
[Hisani]
Picha imetolewa katika “Ecce Homo” ya Antonio Ciseri
-