Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yule Mwanamke Tasa Ashangilia
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Isaya 54:11-

  • Yule Mwanamke Tasa Ashangilia
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.

  • Yule Mwanamke Tasa Ashangilia
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 23. (a) ‘Kufundishwa na Yehova’ kumekuwa na matokeo gani juu ya Wakristo watiwa-mafuta katika siku za mwisho? (b) Watu wa Mungu wamebarikiwa kwa ‘mipaka ya mawe yapendezayo’ katika maana gani?

      23 Mstari wa 13 wa Isaya sura ya 54 unaandaa jibu—wote ‘watafundishwa na Yehova.’ Yesu mwenyewe aliyatumia maneno ya mstari huo kuhusu wafuasi wake watiwa-mafuta. (Yohana 6:45) Nabii Danieli alitabiri kwamba katika huu “wakati wa mwisho,” watiwa-mafuta wangebarikiwa kwa ujuzi mwingi wa kweli na ufahamu wa kiroho wenye kina kirefu. (Danieli 12:3, 4) Ufahamu huo wenye kina kirefu umewawezesha wawe katika mstari wa mbele kuongoza kazi ya uelimishaji iliyo kubwa kupita zote katika historia, wakieneza ufundishaji wa kimungu katika dunia yote. (Mathayo 24:14) Wakati huo huo, ufahamu huo wenye kina kirefu umewasaidia waone tofauti kati ya dini ya kweli na ya uwongo.

  • Yule Mwanamke Tasa Ashangilia
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 24. Tunaweza kuhakikishaje kwamba tunafundishwa na Yehova?

      24 Hivyo, inafaa kila mmoja wetu ajiulize, ‘Je, mimi ninafundishwa na Yehova?’ Hatupokei ufundishaji huo kwa kuketi tu. Ni lazima tutie bidii. Tukilisoma Neno la Mungu kwa ukawaida na kulitafakari, na tukitwaa maagizo kwa kusoma vichapo vyenye msingi wa Biblia vinavyochapishwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” na kujitayarisha kwa ajili ya mikutano ya Kikristo na kuihudhuria, kweli tutafundishwa na Yehova. (Mathayo 24:45-47) Tukijitahidi kutumia yale tunayojifunza na kubaki tukiwa macho na wenye kulinda kiroho, ufundishaji wa kimungu utatutofautisha na wale walio katika ulimwengu huu usiomhofu Mungu. (1 Petro 5:8, 9) Isitoshe, ufundishaji huo utatusaidia ‘kumkaribia Mungu.’—Yakobo 1:22-25; 4:8.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki