Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ujumbe Wenye Tumaini kwa Mateka Walioshuka Moyo
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Tumaini Lisilofaa

      8. Wayahudi wengi wameweka tumaini lao wapi, ijapokuwa wamepewa onyo gani?

      8 Kufikia sasa, Wayahudi wengi hawajamtumainia Yehova kabisa ili wapate wokovu. Kwa mfano, kabla ya Yerusalemu kuanguka, watawala wake walitegemea mataifa yenye nguvu yawaunge mkono, wakawa ni kama wanafanya ukahaba na Misri na Babiloni. (Ezekieli 16:26-29; 23:14) Yeremia alikuwa na sababu nzuri ya kuwaonya hivi: “Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake na moyoni mwake amemwacha BWANA.” (Yeremia 17:5) Lakini watu wa Mungu walifanya vivyo hivyo!

      9. Huenda ikawa Wayahudi wengi ‘wanatoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula’ jinsi gani?

      9 Sasa wamekuwa watumwa wa mojawapo la mataifa waliyokuwa wameyatumainia. Je, wamepata somo? Huenda ikawa wengi hawajapata, kwa maana Yehova anauliza hivi: “Kwani kutoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula? Na mapato yenu kwa kitu kisichoshibisha?” (Isaya 55:2a) Ikiwa Wayahudi mateka wanatumainia mtu mwingine yeyote tofauti na Yehova, ‘wanatoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula.’ Hakika hawatafunguliwa watoke Babiloni kwa sababu desturi ya huko hairuhusu mateka warudi nyumbani kwao. Kwa kweli, Babiloni haiwezi kamwe kuwafaidi Wayahudi wahamishwa kupitia utawala wake wa mabavu, biashara, na ibada ya uongo.

      10. (a) Ikiwa Wayahudi wahamishwa watamsikiliza Yehova, yeye atawathawabishaje? (b) Ni agano gani ambalo Yehova alikuwa amefanya pamoja na Daudi?

      10 Yehova anawasihi sana watu wake hivi: “Nisikilizeni mimi kwa makini, nanyi mtakula vilivyo bora, na kufurahia vinono.

  • Ujumbe Wenye Tumaini kwa Mateka Walioshuka Moyo
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Isaya 55:2b,

  • Ujumbe Wenye Tumaini kwa Mateka Walioshuka Moyo
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Tumaini pekee kwa watu hawa wasiolishwa vizuri kiroho ni Yehova, ambaye sasa anamtumia Isaya kuongea nao kupitia unabii.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki