-
Wageni Wakusanywa Kwenye Nyumba ya Mungu ya SalaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Heri afanyaye haya, na mwanadamu ayashikaye sana; azishikaye sabato asizivunje, auzuiaye mkono wake usifanye uovu wo wote.” (Isaya 56:1, 2)
-
-
Wageni Wakusanywa Kwenye Nyumba ya Mungu ya SalaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
4. Kwa nini kushika Sabato ni muhimu katika Israeli?
4 Unabii huo unakazia kushika Sabato kwa sababu Sabato ni sehemu muhimu ya Sheria ya Kimusa. Kwa kweli, mojawapo ya sababu zinazofanya wakaaji wa Yuda wapelekwe uhamishoni hatimaye ni kwamba wanapuuza Sabato. (Mambo ya Walawi 26:34, 35; 2 Mambo ya Nyakati 36:20, 21) Sabato ni ishara ya uhusiano wa pekee kati ya Yehova na Wayahudi, na wale wanaoishika Sabato wanaonyesha kwamba wanauthamini uhusiano huo. (Kutoka 31:13) Zaidi ya hilo, kuishika Sabato kungewakumbusha watu wa siku za Isaya kwamba Yehova ndiye Muumba. Vilevile kungewakumbusha rehema anazowaonyesha. (Kutoka 20:8-11; Kumbukumbu la Torati 5:12-15) Mwishowe, kuishika Sabato kungeandaa mpangilio mzuri wa kumwabudu Yehova kwa ukawaida. Kwa sababu ya kupumzika mara moja kwa juma bila kufanya kazi yao ya kawaida, wakaaji wa Yuda wangepata nafasi ya kusali, kujifunza, na kutafakari.
5. Kimsingi, Wakristo wanaweza kutumiaje lile shauri la kuishika Sabato?
5 Namna gani Wakristo? Je, kile kitia-moyo cha kuishika Sabato kinawahusu wao pia? La, hakiwahusu moja kwa moja kwa kuwa Wakristo hawako chini ya ile Sheria, na hivyo hawajawekewa takwa la kuishika Sabato. (Wakolosai 2:16, 17) Ingawa hivyo, mtume Paulo alieleza kwamba kuna “pumziko la sabato” kwa ajili ya Wakristo waaminifu. Hilo “pumziko la sabato” linahusu pia kuwa na imani katika dhabihu ya fidia ya Yesu ili kupata wokovu, na kuacha kutegemea matendo peke yake. (Waebrania 4:6-10) Kwa hiyo, maneno ya unabii wa Isaya kuhusu Sabato yanawakumbusha watumishi wa Yehova leo umuhimu wa kuwa na imani katika mpango wa Mungu wa wokovu. Vilevile maneno hayo ni kikumbusha kizuri sana kwamba kuna uhitaji wa kusitawisha uhusiano wa karibu pamoja na Yehova na kuwa wa kawaida katika ibada, bila kigeugeu.
-