-
Wageni Wakusanywa Kwenye Nyumba ya Mungu ya SalaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote.
-
-
Wageni Wakusanywa Kwenye Nyumba ya Mungu ya SalaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Walinzi hao wa kidini hawaelewi mambo, hawafai kuwapa watu walio kama kondoo mwelekezo wa kiroho. Zaidi ya hilo, wao ni wafisadi. Tamaa zao ni za ubinafsi na haziwezi kutoshelezwa. Badala ya kufuata mwelekezo wa Yehova, wanatafuta njia yao wenyewe, wanakimbilia faida isiyo ya haki,
-
-
Wageni Wakusanywa Kwenye Nyumba ya Mungu ya SalaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
22. Viongozi wa kidini wa siku za Yesu wanafananaje na wale wa Yuda ya kale?
22 Pale mwanzoni mwa unabii wake, Isaya alitumia semi kama hizo za mfano kueleza tabia za viongozi wa kidini wa Yuda wasio waaminifu—walilewa, wakasinzia, na kukosa ufahamu kwa njia ya kiroho. Walitwika watu mzigo wa mapokeo ya wanadamu, wakasema uwongo mwingi wa kidini, wakatumainia Ashuru iwasaidie badala ya kumtegemea Mungu. (2 Wafalme 16:5-9; Isaya 29:1, 9-14) Ni wazi kwamba hawajajifunza somo lo lote. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba viongozi wa aina hiyo hiyo ndio waliokuwako karne ya kwanza. Badala ya kuzikubali habari njema walizoletewa na Yesu, Mwana wa Mungu mwenyewe, walimkataa wakatunga hila auawe. Yesu aliwaita “viongozi vipofu” bila kuwaficha, kisha akasema kwamba “ikiwa kipofu aongoza kipofu, wote wawili wataanguka ndani ya shimo.”—Mathayo 15:14.
Walinzi wa Leo
23. Ni unabii gani wa Petro ambao umetimizwa kuhusu viongozi wa kidini?
23 Mtume Petro alionya kwamba walimu wa uwongo pia wangetokea ili kuwapoteza Wakristo. Aliandika hivi: “Kulikuja pia kuwa na manabii wasio wa kweli miongoni mwa watu [wa Israeli], kama pia kutakavyokuwa na walimu wasio wa kweli miongoni mwenu. Hawahawa wataleta ndani kimya-kimya mafarakano yenye kuangamiza na watakana hata mmiliki aliyewanunua, wakijiletea wenyewe uangamizo wa kasi.” (2 Petro 2:1) Matokeo yamekuwa nini kwa sababu ya walimu hao wa uwongo kuleta mafundisho ya uwongo na migawanyiko? Matokeo ni Jumuiya ya Wakristo, ambayo viongozi wake wa kidini leo husali ili Mungu abariki rafiki zao wa kisiasa, kisha wanawaahidi rafiki hao kwamba kuna matazamio mema wakati ujao. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wameonekana wazi kuwa ni vipofu, hawana sauti, tena wamelala usingizi wa kutojali mambo ya kiroho.
-