Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ahuisha Roho ya Wanyenyekevu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 18. Kutukuka kwa Yehova kunaelezwaje, hata hivyo anaonyesha hangaiko gani lenye upendo?

      18 Hapo sasa ndipo nabii Isaya anapoyasimulia maneno yaliyonukuliwa pale mwanzoni: “Yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua [“kuhuisha,” “NW”] roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu [“wanaopondwa,” “NW”].” (Isaya 57:15) Kiti cha ufalme cha Yehova kiko katika mbingu za juu kabisa. Hakuna cheo kingine chochote kilicho juu wala kilichotukuka kuliko hicho. Inafariji kama nini kujua kwamba akiwa huko juu yeye huona kila kitu—si dhambi za waovu tu, bali hata matendo ya haki ya wale wanaojaribu kumtumikia! (Zaburi 102:19; 103:6) Tena, yeye anasikia sauti za kuugua za wale wanaoonewa, na anahuisha mioyo ya waliopondwa. Bila shaka maneno haya yaliigusa mioyo ya Wayahudi waliotubu nyakati za kale. Na hakika yanaigusa mioyo yetu sisi leo.

  • Yehova Ahuisha Roho ya Wanyenyekevu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 21. (a) Yehova alihuishaje roho ya Wakristo watiwa-mafuta mwaka wa 1919? (b) Sisi mmoja-mmoja tunapaswa kusitawisha sifa gani?

      21 Yehova, “yeye aliye juu, aliyetukuka,” aliihangaikia pia hali njema ya mabaki watiwa-mafuta mwaka wa 1919. Kwa sababu ya roho yao ya majuto na unyenyekevu, huyo Mungu mkuu, Yehova, aliwafadhili kwa kuyaona mateso yao na kuwakomboa kutoka katika utekwa wa Kibabiloni.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki