Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ahuisha Roho ya Wanyenyekevu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • ‘Amani Kwao Walio Mbali na Walio Karibu’

      22. Yehova anatabiri wakati gani ujao kwa (a) wenye kutubu? (b) waovu?

      22 Akitofautisha wakati ujao wa wale wanaotubu na wakati ujao wa wale wanaoendelea tu kufuata njia zao za uovu, Yehova anatangaza hivi: “Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; . . . nami nitamponya.

  • Yehova Ahuisha Roho ya Wanyenyekevu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Isaya 57:19

  • Yehova Ahuisha Roho ya Wanyenyekevu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 25. Watu wengi wa mbali na wa karibu huja kujua amani jinsi gani?

      25 Leo, pia, waabudu wa Yehova kila mahali wanatangaza habari njema za Ufalme wa Mungu. Wakristo wa mbali na karibu, katika nchi zaidi ya 230, wanatoa tunda la midomo yao, wakivumisha sifa za yule Mungu mmoja tu wa kweli. Sifa wanazoimba zinasikiwa “tokea mwisho wa dunia.” (Isaya 42:10-12) Wale wanaozisikia semi zao na kuziitikia wanaikubali kweli ya Neno la Mungu, Biblia. Watu wa jinsi hiyo huja kujua amani, inayopatikana kwa kumtumikia “Mungu apaye amani.”—Waroma 16:20.

  • Yehova Ahuisha Roho ya Wanyenyekevu
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 23. Tunda la midomo ni nini, na Yehova ‘anaumbaje’ tunda hilo?

      23 Tunda la midomo ni ile dhabihu ya sifa ambayo hutolewa kuelekea Mungu—tangazo la peupe kuhusu jina lake. (Waebrania 13:15) Yehova ‘anaumbaje’ tangazo hilo la peupe? Ili kutoa toleo la dhabihu ya sifa, ni lazima kwanza mtu ajifunze juu ya Mungu kisha amwamini. Imani, ambayo ni tunda la roho ya Mungu, humchochea mtu huyo awaambie wengine mambo ambayo amesikia. Yaani, yeye hufanya tangazo la peupe. (Waroma 10:13-15; Wagalatia 5:22) Vilevile, na ikumbukwe kwamba Yehova ndiye hasa anayewapa watumishi wake utume wa kutangaza sifa yake. Tena Yehova ndiye anayewakomboa watu wake, na kufanya iwezekane kwao kutoa dhabihu hizo za sifa. (1 Petro 2:9) Kwa hiyo ni sawa kusema kwamba Yehova ndiye anayeumba tunda hilo la midomo.

      24. (a) Ni nani wanaopata kujua amani ya Mungu, na matokeo ni nini? (b) Ni nani ambao hawapati kujua amani, na wanapatwa na matokeo gani?

      24 Lo, Wayahudi wanatoa tunda la midomo lenye kusisimua kama nini wakati wanapoirudia nchi yao wakimwimbia Yehova sifa! Bila shaka wana shangwe ya kuijua amani ya Mungu, hata kama wako “mbali”—mwendo mrefu kutoka Yuda, wakiwa wangali wanangojea kurudi—au wakiwa “karibu,” yaani wakiwa tayari katika nchi yao.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki