Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unafiki Wafichuliwa!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • ndipo utakapojifurahisha katika BWANA; nami nitakupandisha mahali pa nchi palipoinuka; nitakulisha urithi wa Yakobo baba yako; kwa maana kinywa cha BWANA kimenena hayo.”—Isaya 58:13, 14.

  • Unafiki Wafichuliwa!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 19. Ikiwa watu wa Mungu watageuka waanze kushika Sabato, watapata baraka zipi?

      19 Na bado, Wayahudi wakijifunza kutokana na nidhamu hiyo kisha wageuke na kuanza kuuheshimu mpango wa Sabato, watapata baraka nyingi. Matokeo mema ya kufuata ibada ya kweli na kuiheshimu Sabato yatafurika yaenee katika sehemu zote za maisha yao. (Kumbukumbu la Torati 28:1-13; Zaburi 19:7-11) Kwa mfano, Yehova atawafanya watu wake ‘wapande mahali pa nchi palipoinuka.’ Usemi huo unamaanisha kupata usalama na kuwashinda maadui. Yule anayefaulu kusimamia mahali palipoinuka, yaani vilima na milima, ndiye anayefaulu kuisimamia nchi. (Kumbukumbu la Torati 32:13; 33:29) Wakati mmoja Israeli walimtii Yehova, na taifa hilo lilifurahia ulinzi wake na kuheshimiwa, hata kuogopwa, na mataifa mengine. (Yoshua 2:9-11; 1 Wafalme 4:20, 21) Wakimgeukia Yehova tena kwa kumtii, watarudishiwa kiasi fulani cha utukufu huo wa zamani. Yehova atawapa watu wake sehemu kamili ya “urithi wa Yakobo,” yaani zile baraka zilizoahidiwa kupitia agano Lake na baba zao wa zamani, na hasa baraka ya kumiliki Nchi ya Ahadi bila wasiwasi wowote.—Zaburi 105:8-11.

  • Unafiki Wafichuliwa!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Israeli wa Kiroho ‘Apanda Mahali pa Nchi Palipoinuka’

      21, 22. Yehova amefanyaje Israeli wa Mungu ‘apande mahali pa nchi palipoinuka’?

      21 Tangu wakati ambao Wakristo watiwa-mafuta walifunguliwa kutoka katika utekwa wa Kibabiloni mwaka wa 1919, wameadhimisha kwa uaminifu jambo ambalo Sabato ilikuwa kivuli chake. Tokeo ni kwamba, Yehova amewafanya ‘wapande mahali pa nchi palipoinuka.’ Katika maana gani? Kule nyuma mwaka wa 1513 K.W.K., Yehova alifanya agano na wazao wa Abrahamu kwamba, ikiwa wangetii, wangekuwa ufalme wa makuhani na taifa takatifu. (Kutoka 19:5, 6) Yehova aliwabeba wakiwa salama muda wote wa ile miaka 40 ya kuwa jangwani, kama vile tai anavyowabeba makinda wake. Yehova aliwabariki kwa kuwaandalia vitu vingi sana. (Kumbukumbu la Torati 32:10-12) Hata hivyo, taifa hilo halikuwa na imani, na mwishowe lilipoteza mapendeleo yote ambayo lingaliweza kuyapata. Ijapokuwa hivyo, Yehova ana ufalme wa makuhani leo. Ufalme huo ni Israeli wa kiroho wa Mungu.—Wagalatia 6:16; 1 Petro 2:9.

      22 Katika “wakati wa mwisho,” taifa hili la kiroho limefanya jambo lile ambalo Israeli wa kale walishindwa kufanya. Wamedumisha imani yao kwa Yehova. (Danieli 8:17) Wakati washirika wake wanafuata sana viwango vya Yehova vya hali ya juu na njia zake zilizotukuka, Yehova naye anawainua juu katika maana ya kiroho. (Mithali 4:4, 5, 8; Ufunuo 11:12) Kwa kuwa wanalindwa wasipatwe na uchafu unaowazunguka, wanafurahia maisha ya hali ya juu. Na badala ya kufuata njia zao wenyewe tu, wao ‘wanajifurahisha kwa Yehova’ na Neno lake. (Zaburi 37:4) Yehova amewatunza wakawa salama kiroho ijapokuwa wamepingwa vikali ulimwenguni pote. Tangu mwaka wa 1919, “nchi” yao ya kiroho haijaharibiwa hata kidogo. (Isaya 66:8) Wanaendelea kuwa taifa la watu wanaowakilisha jina lake tukufu, wakilitangaza kwa shangwe ulimwenguni kote. (Kumbukumbu la Torati 32:3; Matendo 15:14) Isitoshe, sasa idadi inayoongezeka ya watu watiifu kutoka mataifa yote inashirikiana nao katika pendeleo tukufu la kufundishwa njia za Yehova na kusaidiwa kutembea katika mapito yake.

      23. Ni jinsi gani Yehova ‘amewalisha urithi wa Yakobo’ watumishi wake watiwa-mafuta?

      23 Yehova ‘amewalisha urithi wa Yakobo’ watumishi wake watiwa-mafuta. Isaka alipombariki Yakobo badala ya Esau, maneno ya mzee huyo wa ukoo yalitabiri kwamba wale wote ambao wangedhihirisha imani katika Mbegu iliyoahidiwa ya Abrahamu wangepata baraka nyingi. (Mwanzo 27:27-29; Wagalatia 3:16, 17) Wakristo watiwa-mafuta na waandamani wao ni kama Yakobo, wala si kama Esau, kwani ‘wanathamini mambo matakatifu,’ na hasa chakula cha kiroho ambacho Mungu hugawa kwa wingi. (Waebrania 12:16, 17; Mathayo 4:4) Chakula hiki cha kiroho—kinachohusisha ujuzi wa mambo ambayo Yehova anatimiza kupitia Mbegu iliyoahidiwa, na pia kupitia washirika wa Mbegu hiyo—kinawaimarisha na kuwatia nguvu, tena ni muhimu kwa uhai wao wa kiroho. Basi, ni muhimu sana kwamba waendelee kutwaa lishe ya kiroho daima kwa kusoma Neno la Mungu na kulitafakari. (Zaburi 1:1-3) Ni lazima washirikiane na waamini wenzao kwenye mikutano ya Kikristo. Tena ni jambo la maana sana waunge mkono viwango vya juu vya ibada safi, huku wakiwagawia wengine lishe hiyo kwa shangwe.

      24. Wakristo wa kweli wanaenendaje leo?

      24 Wakristo wa kweli na waendelee kukataa katakata unafiki wa aina zote, huku wakingojea utimizo wa ahadi za Yehova kwa hamu. Wakati wanapolishwa ‘urithi wa Yakobo,’ na waendelee kufurahia usalama wa kiroho wakiwa katika ‘mahali pa nchi palipoinuka.’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki