Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Uwaambie Neno Hili”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • ‘YEHOVA ALINIGUSA KINYWA’

      3. Yehova alifanya jambo gani lisilo la kawaida mwanzoni mwa utume wa Yeremia, naye Yeremia alihisi namna gani?

      3 Kumbuka kwamba mwanzoni wa huduma yake, Yeremia aliambiwa: “Kwa wale wote nitakaokutuma kwao, unapaswa kwenda; na kila jambo nitakalokuamuru, unapaswa kusema. Usiogope kwa sababu ya nyuso zao, kwa maana ‘mimi niko pamoja nawe ili kukukomboa,’ asema Yehova.” (Yer. 1:7, 8) Kisha Mungu akafanya jambo lisilo la kawaida. Yeremia asema: “Yehova akanyoosha mkono wake na kunigusa kinywa changu. Ndipo Yehova akaniambia: ‘Nimeyatia maneno yangu katika kinywa chako. Tazama, nimekupa utume leo.’” (Yer. 1:9, 10) Tangu wakati huo na kuendelea, Yeremia alijua kwamba anazungumza kwa niaba ya Mungu Mweza-Yote.a Kwa msaada wa Mungu, bidii ya Yeremia kwa ajili ya utumishi mtakatifu iliongezeka.—Isa. 6:5-8.

      Picha katika ukurasa wa 34
      Picha katika ukurasa wa 34
      Picha katika ukurasa wa 34

      4. Simulia mifano ya watu wenye bidii ya pekee katika kazi ya kuhubiri.

      4 Leo, Yehova hawagusi kihalisi watumishi wake. Hata hivyo, kupitia roho yake, anawachochea kuwa na tamaa ya kuhubiri habari njema. Wengi wao wana bidii sana.

  • “Uwaambie Neno Hili”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • a Katika kisa hiki, kama ilivyo katika visa vingine vingi, Yehova aliwakilishwa na malaika aliyezungumza kana kwamba ni Yehova mwenyewe.—Amu. 13:15, 22; Gal. 3:19.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki