-
“Uwaambie Neno Hili”Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
‘YEHOVA ALINIGUSA KINYWA’
3. Yehova alifanya jambo gani lisilo la kawaida mwanzoni mwa utume wa Yeremia, naye Yeremia alihisi namna gani?
3 Kumbuka kwamba mwanzoni wa huduma yake, Yeremia aliambiwa: “Kwa wale wote nitakaokutuma kwao, unapaswa kwenda; na kila jambo nitakalokuamuru, unapaswa kusema. Usiogope kwa sababu ya nyuso zao, kwa maana ‘mimi niko pamoja nawe ili kukukomboa,’ asema Yehova.” (Yer. 1:7, 8) Kisha Mungu akafanya jambo lisilo la kawaida. Yeremia asema: “Yehova akanyoosha mkono wake na kunigusa kinywa changu. Ndipo Yehova akaniambia: ‘Nimeyatia maneno yangu katika kinywa chako. Tazama, nimekupa utume leo.’” (Yer. 1:9, 10) Tangu wakati huo na kuendelea, Yeremia alijua kwamba anazungumza kwa niaba ya Mungu Mweza-Yote.a Kwa msaada wa Mungu, bidii ya Yeremia kwa ajili ya utumishi mtakatifu iliongezeka.—Isa. 6:5-8.
4. Simulia mifano ya watu wenye bidii ya pekee katika kazi ya kuhubiri.
4 Leo, Yehova hawagusi kihalisi watumishi wake. Hata hivyo, kupitia roho yake, anawachochea kuwa na tamaa ya kuhubiri habari njema. Wengi wao wana bidii sana.
-
-
“Uwaambie Neno Hili”Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
a Katika kisa hiki, kama ilivyo katika visa vingine vingi, Yehova aliwakilishwa na malaika aliyezungumza kana kwamba ni Yehova mwenyewe.—Amu. 13:15, 22; Gal. 3:19.
-