-
Kaa Macho, Kama Yeremia AlivyofanyaMnara wa Mlinzi—2011 | Machi 15
-
-
10. Kwa nini inaweza kusemwa kwamba mabaki ya watiwa-mafuta wako ‘juu ya mataifa na falme’?
10 Akiwa “Mfalme wa mataifa,” Yehova alimwagiza Yeremia atangaze ujumbe wa hukumu kwa mataifa na falme. (Yer. 10:6, 7) Lakini mabaki ya watiwa-mafuta wako “juu ya mataifa na juu ya falme” katika njia gani? (Yer. 1:10) Kama nabii huyo wa zamani, jamii ya Yeremia imepewa mgawo na Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote mzima. Kwa hiyo, watumishi wa Mungu waliotiwa mafuta wamepewa mamlaka rasmi ya kutangaza ujumbe wa hukumu ulimwenguni pote juu ya mataifa na falme. Wakiwa wamepewa mamlaka na Mungu Aliye Juu Zaidi na wakitumia lugha iliyo wazi ya Neno lake lililoongozwa na roho takatifu, jamii ya Yeremia inatangaza kwamba mataifa na falme za leo zitang’olewa na kuharibiwa kwa njia ya Mungu wakati wake barabara utakapofika. (Yer. 18:7-10; Ufu. 11:18)
-
-
Kaa Macho, Kama Yeremia AlivyofanyaMnara wa Mlinzi—2011 | Machi 15
-
-
14, 15. (a) Kulikuwa na matokeo gani Yeremia aliposhikamana kwa uaminifu na mgawo wake? (b) Watu wa Mungu wanaelewa jambo gani leo kuhusu kazi ya kuhubiri?
14 Yeremia alitangaza bila kuacha ujumbe wa maonyo na hukumu kutoka kwa Yehova, lakini bado alikazia fikira mgawo wake wa “kujenga na kupanda.” (Yer. 1:10) Kazi yake ya kujenga na kupanda ilizaa matunda. Wayahudi fulani na vilevile watu wasio Waisraeli waliokoka kuharibiwa kwa Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K. Tunajua kuhusu Warekabu, Ebed-meleki, na Baruku. (Yer. 35:19; 39:15-18; 43:5-7) Marafiki hao wa Yeremia waliokuwa washikamanifu na wenye kumwogopa Mungu wanafananisha vizuri leo wale walio na tumaini la kuishi duniani ambao wanasitawisha urafiki na jamii ya Yeremia. Jamii ya Yeremia inafurahia sana kuujenga kiroho ‘umati huo mkubwa.’ (Ufu. 7:9) Vivyo hivyo, waandamani hao washikamanifu wa watiwa-mafuta wanafurahi sana kuwasaidia watu wenye mioyo minyoofu kupata ujuzi juu ya kweli.
-