Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ni Fungu Langu
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Septemba 15
    • Watu Mmoja-Mmoja Ambao Yehova Alikuwa Fungu Lao

      8. Eleza tatizo ambalo Asafu alikuwa nalo.

      8 Kwa ujumla, Yehova angekuwa fungu la kabila lote la Walawi. Hata hivyo, ni vizuri kuona kwamba Walawi wakiwa mtu mmoja-mmoja walitumia maneno “Yehova ni fungu langu” ili kuonyesha kwamba walijitoa kwa Mungu na kumtegemea yeye. (Omb. 3:24)

  • Yehova Ni Fungu Langu
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Septemba 15
    • 11. Ni swali gani ambalo Yeremia aliuliza, na lilijibiwa jinsi gani?

      11 Nabii Yeremia ni Mlawi mwingine aliyemwona Yehova kuwa fungu lake. Acheni tuone alichomaanisha alipotumia maneno hayo. Yeremia aliishi huko Anathothi, jiji la Walawi ambalo lilikuwa karibu na Yerusalemu. (Yer. 1:1) Pindi moja, Yeremia alishangaa na kuuliza: Kwa nini waovu walikuwa wakifanikiwa huku waadilifu wakiteseka? (Yer. 12:1) Baada ya kuona mambo yaliyokuwa yakitokea Yerusalemu na Yuda, alihisi kwamba alipaswa ‘kulalamika’ kuhusu mambo aliyoona. Yeremia alijua kwamba Yehova ni mwadilifu. Swali la nabii Yeremia lilijibiwa kwa hakika kupitia mambo ambayo Yehova alimwongoza nabii huyo kutabiri baadaye kwa uwezo wa roho takatifu na jinsi Yehova alivyoyatimiza. Kulingana na unabii mbalimbali kutoka kwa Mungu, wale ambao walitii mwongozo wa Yehova ‘walipata nafsi yao kama nyara,’ lakini watu waovu waliokuwa matajiri walipuuza onyo na kuangamia.—Yer. 21:9.

      12, 13. (a) Ni nini kilichomchochea Yeremia atangaze hivi: “Yehova ni fungu langu,” na alikuwa na mtazamo gani? (b) Kwa nini makabila yote ya Israeli yalihitaji kusitawisha mtazamo wa kungojea?

      12 Baadaye Yeremia alipoangalia nchi yake iliyobaki ukiwa, alihisi kana kwamba alikuwa akitembea katika giza. Ilikuwa ni kana kwamba Yehova alimfanya ‘aketi mahali penye giza kama watu waliokufa zamani.’ (Omb. 1:1, 16; 3:6) Yeremia alikuwa ameliambia taifa hilo lenye kuasi limrudie Baba yao wa mbinguni, lakini ubaya ulikuwa mwingi hivi kwamba Mungu alilazimika kuruhusu Yerusalemu na Yuda kuangamizwa. Yeremia aliumia alipoona hivyo, hata ingawa kosa halikuwa lake. Alipokuwa akiteseka, nabii huyo alikumbuka rehema za Mungu. Alisema hivi: “Hatujaisha.” Kwa kweli, rehema za Yehova ni mpya kila asubuhi! Ndipo Yeremia alipotangaza hivi: “Yehova ni fungu langu.” Aliendelea kuwa na pendeleo la kumtumikia Yehova akiwa nabii.—Soma Maombolezo 3:22-24.

      13 Kwa miaka 70, Waisraeli hawangekuwa na nchi yao. Ingeachwa ukiwa. (Yer. 25:11) Lakini maneno “Yehova ni fungu langu” yaliyosemwa na Yeremia yalionyesha alikuwa na uhakika kwamba Mungu angewarehemu, na hilo lilimpa sababu ya kuwa na “mtazamo wa kungojea.” Makabila yote ya Israeli yalikuwa yamepoteza urithi wao, hivyo yalihitaji kusitawisha mtazamo kama wa nabii huyo. Yehova peke yake ndiye aliyekuwa tumaini lao. Baada ya miaka 70, watu wa Mungu walirudishwa katika nchi yao na wakapata pendeleo la kumtumikia huko.—2 Nya. 36:20-23.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki