-
Wakati wa Kuja Kwa Mesiya WafunuliwaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
Gabrieli amwambia Danieli hivi: “Muda wa majuma sabini umeamriwa juu ya watu wako, na juu ya mji wako mtakatifu, ili kukomesha makosa, na kuishiliza dhambi, na kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, na kuleta haki ya milele, na kutia muhuri maono na unabii, na kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu [“mahali patakatifu kabisa,” BHN].
-
-
Wakati wa Kuja Kwa Mesiya WafunuliwaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
Hilo lingetukia mnamo “majuma sabini.” Kwa kuwa Gabrieli hataji siku, hayo si majuma yenye siku saba kila moja, ambayo yangejumlika kuwa siku 490—mwaka mmoja na miezi minne tu. Kule kujengwa upya kulikotabiriwa kwa Yerusalemu “pamoja na njia kuu zake na handaki” kulichukua muda mrefu kuliko huo. Majuma hayo ni majuma ya miaka. Tafsiri kadhaa za kisasa zadokeza kwamba kila juma lina urefu wa miaka saba. Kwa kielelezo, kwenye Danieli 9:24, Biblia Habari Njema husema: “Miaka saba mara sabini.”
-
-
Wakati wa Kuja Kwa Mesiya WafunuliwaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
Kwa kupendeza, The Revised English Bible husema hivi: “Miaka sabini mara saba imewekwa kwa ajili ya watu wako na jiji lako takatifu.” Baada ya uhamisho na kuteseka huko Babiloni kwa miaka 70, Wayahudi wangepata upendeleo wa pekee kutoka kwa Mungu kwa miaka 490, au miaka 70 mara 7.
-