Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho Wao
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • VITA YA MWISHO

      20. Malaika afafanuaje vita ya mwisho ya mfalme wa kaskazini?

      20 Ushindani kati ya mfalme wa kaskazini na mfalme wa kusini—uwe wa kijeshi, kiuchumi, au mwingineo wowote—wakaribia kwisha. Akifunua kinaganaga juu ya pambano lililo mbele, malaika wa Yehova asema hivi: “Habari zitokazo mashariki [“macheo ya jua,” NW] na kaskazini zitamfadhaisha [mfalme wa kaskazini]; naye atatoka kwa ghadhabu nyingi, ili kuharibu, na kuwaondolea mbali watu wengi.

  • Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho Wao
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • —Danieli 11:44, 45.

      21. Kuna mambo gani bado ya kujifunza juu ya mfalme wa kaskazini?

      21 Muungano wa Sovieti ulipovunjika Desemba 1991, mfalme wa kaskazini alipatwa na madhara makubwa. Ni nani atakayekuwa mfalme huyo wakati ambapo Danieli 11:44, 45 litakapotimizwa? Je, atakuwa mojawapo ya nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti? Au atabadilika kabisa, kama vile ambavyo amefanya mara kadhaa? Je, kutengenezwa kwa silaha za nyuklia kunakofanywa na mataifa mengine katika shindano jingine la silaha kutabadili utambulisho wa mfalme huyo? Wakati tu ndio utakaotoa majibu ya maswali hayo. Ni jambo la hekima kwamba tusikisie-kisie. Mfalme wa kaskazini arudiapo vita yake ya mwisho, wale wote wenye ufahamu wa kina unaotegemea Biblia watauona utimizo wa unabii huo waziwazi.—Ona “Wafalme Katika Danieli Sura ya 11,” kwenye ukurasa wa 284.

      22. Ni maswali gani yanayozuka juu ya shambulio la mwisho la mfalme wa kaskazini?

      22 Hata hivyo, twajua hatua ambayo mfalme wa kaskazini atachukua hivi karibuni. Akichochewa na ‘habari zitokazo macheo ya jua na kaskazini,’ atapanga vita ili “kuwaondolea mbali watu wengi.” Vita hiyo itapiganwa dhidi ya nani? Nazo ni “habari” gani zinazochochea shambulio hilo?

      ASHTUSHWA NA HABARI ZENYE KUSUMBUA

      23. (a) Ni tukio gani lenye kutokeza ambalo lazima litukie kabla ya Har–Magedoni? (b) “Wafalme watokao macheo ya jua” ni akina nani?

      23 Fikiria jambo ambalo kitabu cha Ufunuo chasema juu ya mwisho wa Babiloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli. Kabla ya “vita ya siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote,” Har–Magedoni, adui huyo mkubwa wa ibada ya kweli “atachomwa kabisa kwa moto.” (Ufunuo 16:14, 16; 18:2-8) Kuharibiwa kwake kuliwakilishwa na kumwagwa kwa bakuli la sita la hasira ya kisasi ya Mungu kwenye mto wa ufananisho wa Eufrati. Mto huo wakauka ili “njia ipate kutayarishwa kwa ajili ya wafalme watokao macheo ya jua.” (Ufunuo 16:12) Wafalme hao ni nani? Si wengine ila Yehova Mungu na Yesu Kristo!—Linganisha Isaya 41:2; 46:10, 11.

      24. Ni tendo gani la Yehova ambalo huenda likamsumbua mfalme wa kaskazini?

      24 Kuharibiwa kwa Babiloni Mkubwa kwafafanuliwa kinaganaga kwenye kitabu cha Ufunuo, kinachotaarifu hivi: “Pembe kumi ulizoziona [wafalme wanaotawala katika wakati wa mwisho], na hayawani-mwitu [Umoja wa Mataifa], hawa watamchukia kahaba na watamfanya ukiwa na kuwa uchi, na watakula kabisa sehemu zake zenye nyama na watamchoma kabisa kwa moto.” (Ufunuo 17:16) Kwa nini wafalme watamharibu Babiloni Mkubwa? Kwa sababu ‘Mungu atia ndani ya mioyo yao ili watekeleze fikira yake.’ (Ufunuo 17:17) Mfalme wa kaskazini ni mmoja wa watawala hao. Huenda habari asikiazo kutoka “macheo ya jua” zarejezea tendo hilo la Yehova, atiapo ndani ya mioyo ya viongozi wa kibinadamu fikira ya kumwangamiza kahaba huyo mkubwa wa kidini.

  • Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho Wao
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • 26. Kama inavyoonyeshwa na unabii wa Ezekieli, huenda habari ‘itokayo kaskazini’ yatokana na nani?

      26 Ezekieli, aliyeishi wakati mmoja na Danieli, alitabiri pia juu ya shambulio dhidi ya watu wa Mungu “katika siku za mwisho.” Alisema kwamba uhasama huo ungeanzishwa na Gogu wa Magogu, yaani, Shetani Ibilisi. (Ezekieli 38:14, 16) Kwa njia ya kitamathali, Gogu atokea upande gani? “Pande za mwisho za kaskazini,” asema Yehova, kupitia Ezekieli. (Ezekieli 38:15) Hata shambulio hilo liwe kali namna gani, halitawaharibu watu wa Yehova. Tukio hilo lenye kutokeza litamfanya Yehova achukue hatua ili kuyaangamiza majeshi ya Gogu. Kwa hiyo, Yehova amwambia Shetani hivi: ‘Nitakutia kulabu katika mataya yako, nami nitakutoa.’ “Nitakupandisha toka pande za mwisho za kaskazini; nami nitakuleta juu ya milima ya Israeli.” (Ezekieli 38:4; 39:2) Kwa hiyo, habari ‘itokayo kaskazini’ ambayo yamkasirisha mfalme wa kaskazini lazima iwe yatokana na Yehova. Lakini Mungu tu ndiye atakayeamua habari kamili zitokazo ‘macheo ya jua na kaskazini’ zitakuwa nini, nao wakati utafunua.

      27. (a) Kwa nini Gogu atayachochea mataifa, kutia ndani mfalme wa kaskazini, yashambulie watu wa Yehova? (b) Matokeo ya shambulio la Gogu yatakuwa nini?

      27 Gogu anapanga shambulio la kufa na kupona dhidi ya ufanisi wa “Israeli wa Mungu,” ambao, pamoja na “umati mkubwa” wa “kondoo wengine,” si sehemu ya ulimwengu wake. (Wagalatia 6:16; Ufunuo 7:9; Yohana 10:16; 17:15, 16; 1 Yohana 5:19) Gogu awatazama kichongochongo “watu waliokusanyika toka mataifa, waliopata ng’ombe na mali [za kiroho].” (Ezekieli 38:12) Akiyaona makazi ya kiroho ya Wakristo kuwa “nchi yenye vijiji visivyo na maboma” iliyo rahisi kuteka, Gogu ajitahidi sana kufagilia mbali kipingamizi hicho apate kudhibiti kabisa wanadamu. Lakini ashindwa. (Ezekieli 38:11, 18; 39:4) Wafalme wa dunia, kutia ndani mfalme wa kaskazini, washambuliapo watu wa Yehova, ‘watakuwa wamefikia kikomo chao.’

      ‘MFALME ATAKUWA AMEFIKIA KIKOMO CHAKE’

      28. Twajua nini juu ya wakati ujao wa mfalme wa kaskazini na mfalme wa kusini?

      28 Vita ya mwisho ya mfalme wa kaskazini haitakuwa dhidi ya mfalme wa kusini. Kwa hiyo, mfalme wa kaskazini hafikii kikomo chake mikononi mwa mpinzani wake mkuu. Hali kadhalika, mfalme wa kusini haharibiwi na mfalme wa kaskazini. Mfalme wa kusini aharibiwa, “bila kazi ya mikono” ya kibinadamu, bali na Ufalme wa Mungu.a (Danieli 8:25) Kwa hakika, kwenye vita ya Har–Magedoni, wafalme wote wa kidunia wataondolewa na Ufalme wa Mungu, na yaonekana hilo ndilo litakalompata mfalme wa kaskazini. (Danieli 2:44) Andiko la Danieli 11:44, 45 lafafanua matukio yanayoelekeza kwenye pigano la mwisho. Si ajabu basi kwamba “hakuna atakayemsaidia”!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki