Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuwatambua Waabudu wa Kweli Katika Wakati wa Mwisho
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • FURAHA YA WATAKATIFU

      24, 25. (a) Ni kipindi gani cha wakati kinachotabiriwa kwenye Danieli 12:12, na yaonekana kilianza lini na kukoma lini? (b) Mabaki ya watiwa-mafuta walikuwa na hali gani ya kiroho mwanzoni mwa zile siku 1,335?

      24 Malaika wa Yehova amalizia unabii wake kuhusu watakatifu kwa maneno haya: “Heri [“Mwenye furaha ni yule,” NW] angojaye, na kuzifikilia [“kuzitarajia,” NW] siku hizo elfu na mia tatu na thelathini na tano.” (Danieli 12:12) Malaika hadokezi jambo lolote juu ya wakati ambapo kipindi hicho huanza au kumalizika. Historia yadokeza kwamba chafuatia karibu-karibu kile kipindi kilichokitangulia. Kwa hiyo, kingeanza vuli ya 1922 hadi mwisho-mwisho wa masika ya 1926 (kwenye Kizio cha Kaskazini). Je, watakatifu walifurahi mwishoni mwa kipindi hicho? Naam, katika njia muhimu za kiroho.

      25 Hata baada ya mkusanyiko mwaka wa 1922 (unaoonyeshwa kwenye ukurasa wa 302), baadhi ya watakatifu wa Mungu wangali walikuwa wakitamani nyakati zilizopita. Bado chanzo chao cha msingi cha habari za kujifunza kwenye mikutano kilikuwa Biblia na yale mabuku ya Studies in the Scriptures, yaliyoandikwa na C. T. Russell. Wakati huo, watu wengi walikuwa na maoni ya kwamba mwaka wa 1925 ndio mwaka ambao ufufuo ungeanza na Paradiso ingerejeshwa duniani. Kwa hiyo, wengi walitumikia wakiwa na tarehe fulani hususa akilini. Wengine walikataa kwa kiburi kushiriki katika kazi ya kuhubiria watu. Hali hiyo haikuwa yenye kufurahisha.

      26. Zile siku 1,335 zilipokuwa zikiendelea, hali ya kiroho ya watiwa-mafuta ilibadilikaje?

      26 Hata hivyo, zile siku 1,335 zilipoendelea, mambo yakaanza kubadilika. Kuhubiri kukatangulizwa, huku mipango ikifanywa ili kila mtu ashiriki katika huduma ya shambani. Mipango ilifanywa ili watu wajifunze The Watch Tower kwenye mikutano kila juma. Makala ya Machi 1, 1925, ilikuwa na makala ya kihistoria yenye kichwa “Kuzaliwa kwa Taifa,” ikiwaelewesha kikamili watu wa Mungu juu ya mambo yaliyotukia kipindi cha kati ya 1914 na 1919. Baada ya mwaka wa 1925 kupita, watakatifu hawakuendelea kumtumikia Mungu wakiwa na tarehe hususa akilini. Badala yake, kutakaswa kwa jina la Yehova kulikuwa jambo la kutangulizwa. Kweli hiyo muhimu ilikaziwa, kuliko wakati mwingine wowote, katika makala ya gazeti Watch Tower la Januari 1, 1926, yenye kichwa “Ni Nani Atakayemheshimu Yehova?” Kwenye mkusanyiko katika Mei 1926, kitabu Deliverance kilitolewa. (Ona ukurasa wa 302.) Hicho kilikuwa kitabu kimoja katika mfululizo wa vitabu vilivyokusudiwa kuchukua mahali pa Studies in the Scriptures. Watakatifu waliacha kutazama nyuma. Walikuwa wakitazamia kwa uhakika wakati ujao na kazi iliyokuwa mbele yao. Kwa hiyo, kama ilivyotabiriwa zile siku 1,335 zilikoma watakatifu wakiwa na furaha.

      27. Kuchunguza Danieli sura ya 12 hutusaidiaje kuwatambua kabisa watiwa-mafuta wa Yehova?

      27 Bila shaka, si wote waliovumilia kipindi hicho chenye msukosuko. Hapana shaka kwamba ndiyo sababu iliyomfanya malaika akazie umuhimu wa “kuzitarajia.” Wale waliovumilia na kuendelea kuwa na matarajio walibarikiwa sana. Kuchunguza Danieli sura ya 12 kwadhihirisha hilo. Kama ilivyotabiriwa, watiwa-mafuta walifufuliwa kiroho. Walipewa ufahamu wenye kina wa pekee wa Neno la Mungu, wakiwezeshwa ‘kwenda mbio huko na huko’ katika hilo, wakiongozwa na roho takatifu, na kufunua mambo ambayo yamekuwa mafumbo kwa muda mrefu. Yehova aliwatakasa na kuwafanya wang’ae kiroho, wakiwa waangavu kama nyota. Kwa hiyo, waliwasaidia wengi wawe na msimamo wenye uadilifu mbele za Yehova Mungu.

  • Kuwatambua Waabudu wa Kweli Katika Wakati wa Mwisho
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • Siku 1,335: Septemba 1922 hadi Mei 1926

      Danieli 12:12 (Wakristo watiwa-mafuta

      wafurahi.)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki