-
Aokolewa Asiliwe na Simba!Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
16. (a) Kwa nini Dario alimheshimu Mungu wa Danieli? (b) Dario alikuwa na matumaini gani kuhusu Danieli?
16 Dario alihisi kwamba hana la kufanya kuhusu hilo. Sheria haingeweza kutanguliwa, wala “kosa” la Danieli halingeweza kusamehewa. Dario angeweza tu kumwambia Danieli “Mungu wako unayemtumikia daima, yeye atakuponya.” Yaonekana Dario alimheshimu Mungu wa Danieli. Yehova ndiye aliyekuwa amempa Danieli uwezo wa kutabiri kuanguka kwa Babiloni. Pia Mungu alikuwa amempa Danieli “roho bora,” iliyomtofautisha na wale mawaziri wengine. Huenda Dario alijua kwamba makumi ya miaka mapema, Mungu huyohuyo alikuwa amewaokoa vijana watatu Waebrania wasiteketee kwenye tanuru ya moto. Yamkini, mfalme alitumaini kwamba Yehova angemwokoa Danieli, kwa kuwa Dario hangeweza kubadili sheria aliyokuwa ametia sahihi. Basi, Danieli akatupwa katika tundu la simba.c
-
-
Aokolewa Asiliwe na Simba!Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
c Huenda tundu hilo la simba lilikuwa shimo la chini ya ardhi lenye mdomo upande wa juu. Huenda pia lilikuwa na milango au viunzi vya chuma ambavyo vingeweza kuinuliwa ili kuruhusu wanyama waingie.
-