-
“Njia za Yehova Zimenyooka”Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 15
-
-
9, 10. Andiko la Hosea 11:1-4 liliwahusuje Waisraeli?
9 Tunaweza kuwa na uhakika kwamba sikuzote Yehova huwatendea watu wake kwa upendo. Uthibitisho wa jambo hilo unapatikana katika Hosea 11:1-4,
-
-
“Njia za Yehova Zimenyooka”Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 15
-
-
Nilizidi kuwavuta kwa kamba za mtu wa udongo, kwa kamba za upendo, hata nikawa kwao kama wale wanaoondoa nira kwenye mfupa wa mataya yao, nami kwa upole nikamletea kila mmoja wao chakula.”
10 Katika andiko hilo, Waisraeli wanalinganishwa na mtoto mchanga. Yehova aliwafundisha Waisraeli kutembea, akawachukua mikononi mwake. Naye alizidi kuwavuta kwa “kamba za upendo.” Mfano huo unavutia kama nini! Wazia kwamba wewe ni mzazi nawe unamsaidia mtoto wako mchanga atembee kwa mara ya kwanza. Unanyoosha mikono yako. Huenda ukatumia kamba ili mtoto wako aishike, asije akaanguka. Naam, hivyo ndivyo Yehova anavyokupenda sana. Anafurahi kukuongoza kwa “kamba za upendo.”
11. Ni kwa njia gani Mungu ‘alikuwa kama mtu anayeondoa nira’?
11 Yehova aliposhughulika na Waisraeli, ‘alikuwa kwao kama wale wanaoondoa nira kwenye mfupa wa mataya yao, naye kwa upole akamletea kila mmoja wao chakula.’ Mungu alikuwa kama mtu anayeondoa nira au kuirudisha nyuma mbali vya kutosha ili kumwezesha mnyama ale kwa starehe. Waisraeli walipovunja nira ya ujitiisho kwa Yehova ndipo walipotiwa chini ya nira yenye kukandamiza ya adui zao. (Kumbukumbu la Torati 28:45, 48; Yeremia 28:14) Na tusianguke kamwe mikononi mwa adui wetu mkuu, Shetani, ili nira yake yenye kukandamiza isije ikatuumiza. Badala yake, acheni tuendelee kutembea kwa ushikamanifu pamoja na Mungu wetu mwenye upendo.
-