-
“Tangazeni Mambo Haya Kati ya Mataifa”Izingatie Siku ya Yehova Maishani
-
-
Ungetendaje ikiwa ungemsikia simba akinguruma?
1. Kwa nini twaweza kusema kwamba Yehova anaposema na nabii wake ni kama simba anaponguruma?
JE, UMEWAHI kumsikia simba akinguruma? Simba hunguruma kwa sauti yenye kuogopesha sana. Mngurumo wake unaweza kusikika umbali wa kilometa nane hivi. Ungefanya nini ikiwa usiku fulani mtulivu ungemsikia simba akinguruma karibu nawe? Huenda ungechukua hatua mara moja. Amosi, mmoja wa wale manabii 12 ambao tunachunguza maandishi yao, alitumia mfano huu: “Kuna simba ambaye amenguruma! Ni nani hataogopa? Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova mwenyewe amesema! Ni nani ambaye hatatoa unabii?” (Amosi 3:3-8) Ikiwa ungemsikia Yehova mwenyewe akizungumza, je, hungechukua hatua kama alivyofanya Amosi? Amosi alichukua hatua mara moja ya kutoa unabii dhidi ya taifa la Israeli la makabila kumi.
-
-
“Tangazeni Mambo Haya Kati ya Mataifa”Izingatie Siku ya Yehova Maishani
-
-
3. Unaweza kushirikije katika kazi kama ile iliyofanywa na wale manabii ambao tunajifunza vitabu vyao?
3 Je, kweli unashiriki katika kazi kama ile iliyofanywa na manabii? Huenda hujapata kumsikia simba akinguruma katika maana ya kwamba hujapuliziwa moja kwa moja na Yehova. Hata hivyo, katika Neno lake Biblia, umesikia ujumbe muhimu kuhusu siku ya Yehova inayokaribia.
-