-
Jitahidi Kuwaona Wengine Kama Yehova AnavyowaonaMnara wa Mlinzi—2003 | Machi 15
-
-
Siku moja, Yehova alimwagiza Yona aondoke Israeli na kusafiri kwenda Ninawi, mji mkuu wa Milki ya Ashuru yenye nguvu. Alipewa mgawo gani? Akawaonye Waninawi kwamba mji wao mkubwa ungeharibiwa. (Yona 1:1, 2)
-
-
Jitahidi Kuwaona Wengine Kama Yehova AnavyowaonaMnara wa Mlinzi—2003 | Machi 15
-
-
6. Kwa nini Yehova alimchagua Yona kwenda Ninawi?
6 Ni nini huja akilini mwako unapomfikiria Yona? Je, unamwona kuwa nabii asiyetii? Maoni ya kijuujuu yanaweza kufanya ufikiri alikuwa nabii asiyetii. Bila shaka, Mungu hangemchagua nabii asiyetii. Ni lazima Yona awe alikuwa na sifa fulani nzuri. Fikiria sifa zake akiwa nabii.
7. Yona alimtumikia Yehova chini ya hali gani huko Israeli, na kufahamu hilo kunaathirije maoni yako kumhusu?
7 Yona alikuwa amefanya kazi ngumu kwa uaminifu huko Israeli, eneo lisilokuwa na matokeo. Nabii Amosi aliyeishi karibu wakati mmoja na Yona, alisema kwamba siku hizo Waisraeli walipenda vitu vya kimwili na anasa.b Uovu ulikuwa umeenea sana nchini, lakini Waisraeli hawakujali hata kidogo. (Amosi 3:13-15; 4:4; 6:4-6) Hata hivyo, Yona aliendelea kwa uaminifu na mgawo wake wa kuwahubiria. Ikiwa wewe ni mhubiri wa habari njema, unajua jinsi ilivyo vigumu kuzungumza na watu ambao wameridhika na maisha na wasiojali. Hivyo basi, ingawa Yona alikuwa na udhaifu, tusisahau uaminifu wake na uvumilivu wake alipowahubiria Waisraeli wasio na imani.
8. Ni magumu gani ambayo yangemkabili nabii Mwisraeli huko Ninawi?
8 Mgawo wake wa kwenda Ninawi ulikuwa mgumu hata zaidi. Ili kufika kwenye jiji hilo, Yona alilazimika kutembea umbali wa kilometa 800 hivi, safari yenye kuchosha ambayo ingechukua angalau muda wa mwezi mmoja. Akiwa huko, nabii huyo angelazimika kuwahubiria Waashuru waliokuwa wakatili. Mara nyingi vita vyao vilitia ndani mateso ya kinyama. Hata walijivunia ukatili wao. Si ajabu kwamba Ninawi uliitwa “mji wa damu”!—Nahumu 3:1, 7.
-