-
Watu wa Yehova Waliorudishwa Wamsifu Duniani PoteMnara wa Mlinzi—2001 | Februari 15
-
-
10, 11. Unabii wa Sefania wa kurudishwa ungetimizwa lini kwa njia kubwa, nasi twajuaje hilo?
10 Kurudishwa kwingine kulitukia katika karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida, wakati ambapo Yesu Kristo alikusanya mabaki ya Israeli waingie katika ibada ya kweli. Kurudishwa huko kuliashiria mambo ambayo bado yangekuja, kwa kuwa utimizo mkubwa zaidi wa kurudishwa ungetukia wakati ujao. Unabii wa Mika ulitabiri hivi: “Lakini itakuwa katika siku za mwisho, ya kwamba mlima wa nyumba ya BWANA [“Yehova,” NW] utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na watu wa mataifa watauendea makundi makundi.”—Mika 4:1.
11 Hilo lingetukia lini? Kama unabii ulivyosema, jambo hilo lingetukia katika “siku za mwisho”—naam wakati wa ‘siku hizi za mwisho.’ (2 Timotheo 3:1)
-
-
Watu wa Yehova Waliorudishwa Wamsifu Duniani PoteMnara wa Mlinzi—2001 | Februari 15
-
-
12. Ibada ya kweli imekwezwaje katika siku hizi za mwisho?
12 Kwa hiyo, katika siku hizi za mwisho, “mlima wa nyumba ya Yehova u[me]wekwa imara juu ya vilima.” Ibada ya kweli ya Yehova iliyoinuka sana imerudishwa, ikafanywa imara, na kukwezwa juu ya aina nyingine zote za dini. Kama unabii wa Mika ulivyotabiri tena, “watu wa mataifa watauendea makundi makundi.”
-
-
Watu wa Yehova Waliorudishwa Wamsifu Duniani PoteMnara wa Mlinzi—2001 | Februari 15
-
-
13, 14. “Siku za mwisho” za ulimwengu huu zilianza lini, na tangu wakati huo ni nini ambacho kimekuwa kikiendelea kuhusiana na ibada ya kweli?
13 Matukio yanayotimiza unabii wa Biblia yathibitisha kwamba “siku za mwisho” za ulimwengu huu zilianza mwaka wa 1914. (Marko 13:4-10) Historia yaonyesha kwamba Yehova alianza kukusanya tena mabaki waaminifu wa watiwa-mafuta waliokuwa na tumaini la kimbingu, waingie katika ibada ya kweli. Halafu, “umati mkubwa . . . kutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha”—watu walio na tumaini la kuishi milele duniani umekuwa ukikusanywa.—Ufunuo 7:9.
14 Tangu Vita ya Ulimwengu ya Kwanza hadi leo, ibada ya Yehova inayotolewa na wale wanaoitwa kwa jina lake, imesonga mbele sana chini ya mwelekezo wake. Tangu baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza hadi sasa, idadi ya waabudu wa Yehova imeongezeka tokea maelfu machache ya watu na kufikia karibu watu milioni sita, wanaokusanywa katika makutaniko yapatayo 91,000 katika nchi 235. Kila mwaka, watangazaji hawa wa Ufalme hutumia muda wa zaidi ya saa bilioni moja wakimsifu Mungu hadharani. Ni wazi kwamba Mashahidi hao wa Yehova ndio wanaotimiza maneno ya Yesu ya unabii: “Na habari njema hii ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo mwisho utakapokuja.”—Mathayo 24:14.
-