-
“Mikono Yako Isilegee”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
Kwanza, ni lazima tujihadhari tusiwe kama Wayahudi katika siku ya Sefania walioacha kumfuata Yehova kwa sababu walitilia shaka ukaribu wa siku ya Yehova. Si lazima kwamba Wayahudi hawa walitaja waziwazi shaka zao, lakini mwendo waliochukua ulifunua kwamba wao kwa kweli hawakuamini kwamba siku ya Yehova iliyo kuu ilikuwa karibu. Wao walikazia akili kurundika mali badala ya kufuliza kumtarajia Yehova.—Sefania 1:12, 13; 3:8.
14 Leo si wakati wa kuacha shaka zikue mioyoni mwetu. Halingekuwa jambo la hekima kuahirisha akilini au moyoni kuja kwa siku ya Yehova. (2 Petro 3:1-4, 10) Twapaswa kuepuka kuacha kumtumikia Yehova au ‘kulegea mikono’ katika utumishi wake. Hilo latia ndani ‘kutofanya mambo kwa mkono mlegevu’ katika kuhubiri “habari njema.”—Mithali 10:4; Marko 13:10, NW.
-
-
“Mikono Yako Isilegee”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
Kupambana na Kutojali
15. Ni nini kiwezacho kutufanya tukose bidii katika utumishi wa Yehova, na tatizo hilo lilitabiriwaje katika unabii wa Sefania?
15 Pili, twapaswa kulinda dhidi ya matokeo yenye kudhoofisha ya kutojali. Katika nchi nyingi za Magharibi, kutojali mambo ya kiroho kwaweza kusababisha kuvunjika moyo miongoni mwa wahubiri fulani wa habari njema. Hali kama hiyo ya kutojali ilikuwapo katika siku ya Sefania. Yehova alisema hivi kupitia nabii wake: “Nitawaadhibu watu . . . wasemao katika mioyo yao, BWANA hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.” (Sefania 1:12) Akiandika kuhusu fungu hili katika Cambridge Bible for Schools and Colleges, A. B. Davidson alisema kwamba hilo fungu larejezea watu waliokuwa “wameshindwa na kutojali kabisa au hata kushindwa na hali ya kutoamini kwamba kuna uwezo wa juu zaidi utakaoingilia mambo ya wanadamu.”
-