-
Siku ya Hukumu ya Yehova I Karibu!Mnara wa Mlinzi—2001 | Februari 15
-
-
14. Mungu angewachunguza kwa undani kadiri gani wale wanaodai kuwa waabudu wake?
14 Yehova angewachunguza kwa undani kadiri gani wale wanaodai kuwa wanamwabudu? Unabii huo waendelea kusema hivi: “Kisha itakuwa wakati ule, nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami nitawaadhibu watu walioganda juu ya sira zao; wasemao katika mioyo yao, BWANA hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.
-
-
Siku ya Hukumu ya Yehova I Karibu!Mnara wa Mlinzi—2001 | Februari 15
-
-
15. (a) Ni nini ambacho kingewapata makuhani waasi-imani wa Yerusalemu? (b) Ni nini kitakachowapata waabudu wa dini isiyo ya kweli leo?
15 Makuhani waasi-imani wa Yerusalemu walikuwa wakichanganya ibada ya Yehova na dini isiyo ya kweli. Ingawa waliona wako salama, Mungu angewatafuta kwa taa ambazo zingeangaza katika giza la kiroho ambamo wamejificha. Hakuna yeyote ambaye angeponyoka kutangazwa na kutekelezwa kwa hukumu ya Mungu. Waasi-imani hao wasiojali walikuwa wametulia kama sira ndani ya pipa la divai. Hawakutaka kusumbuliwa na tangazo lolote la kuingiliwa na Mungu katika shughuli za wanadamu, lakini hawangeponyoka hukumu ya Mungu dhidi yao. Pia, waabudu wa dini isiyo ya kweli leo, kutia ndani wafuasi wa Jumuiya ya Wakristo hali kadhalika wale ambao wameasi ibada ya Yehova, hawataponyoka. Wakikana kwamba hizi si “siku za mwisho,” wanasema moyoni mwao, “BWANA hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.” Lakini wamekosea kama nini!—2 Timotheo 3:1-5; 2 Petro 3:3, 4, 10.
-