-
Yehova Hutoa Amani na Kweli kwa WingiMnara wa Mlinzi—1996 | Januari 1
-
-
‘Nitakuwa na Wivu kwa Ajili ya Sayuni’
6, 7. Ni katika njia gani Yehova alikuwa ‘mwenye wivu kwa ajili ya Sayuni kwa ghadhabu kuu’?
6 Usemi huo watokea mara ya kwanza kwenye Zekaria 8:2, ambapo twasoma hivi: ‘BWANA wa majeshi asema hivi, Mimi nitakuwa na wivu kwa ajili ya Sayuni, wivu mkuu, nami nitakuwa na wivu kwa ajili yake kwa ghadhabu kuu.’ Ahadi ya Yehova ya kuwa mwenye wivu, kuwa na bidii sana, kwa ajili ya watu wake ilimaanisha kwamba angekuwa macho ili awarudishie amani. Kurudishwa kwa Israeli katika bara lalo na kujengwa upya kwa hekalu kulikuwa uthibitisho wa bidii hiyo.
7 Lakini, vipi juu ya wale ambao walikuwa wamepinga watu wa Yehova? Bidii yake kwa ajili ya watu wake ingetoshana na ‘ghadhabu yake kuu’ juu ya maadui wake. Wayahudi waaminifu walipoabudu kwenye hekalu lililojengwa upya, wangeweza kufikiria yale yaliyopata Babiloni lenye nguvu, ambalo sasa lilikuwa limeanguka. Pia waliweza kufikiria juu ya kushindwa kabisa kwa maadui waliojaribu kuzuia kujengwa upya kwa hekalu. (Ezra 4:1-6; 6:3) Nao waliweza kumshukuru Yehova kwamba alikuwa ametimiza ahadi yake. Bidii yake iliwaletea ushindi!
-
-
Yehova Hutoa Amani na Kweli kwa WingiMnara wa Mlinzi—1996 | Januari 1
-
-
9. Ni badiliko gani la hali lenye kutokeza lililopatwa na “Israeli wa Mungu” katika 1919?
9 Ingawa matangazo hayo mawili yalikuwa na umaana katika Israeli la kale, hayo pia yana umaana sana kwetu sisi wakati karne hii ya 20 iendeleapo kumalizika. Karibu miaka 80 iliyopita, wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, maelfu machache ya watiwa-mafuta ambao wakati huo waliwakilisha “Israeli wa Mungu” walienda katika utekwa wa kiroho, kama tu Israeli la kale lilivyoenda katika utekwa Babiloni. (Wagalatia 6:16) Kiunabii, wao walifafanuliwa kuwa maiti zenye kulala barabarani. Na bado, wao walikuwa na tamaa yenye unyoofu ya kumwabudu Yehova “katika roho na kweli.” (Yohana 4:24) Hivyo, katika 1919, Yehova aliwafungua kutoka utekwani, akiwainua kutoka kwa hali yao ya kuwa wafu kiroho. (Ufunuo 11:7-13) Hivyo, Yehova alijibu kwa Ndiyo kubwa sana swali hili la kiunabii la Isaya: “Je, kweli bara litazaliwa kwa utungu katika siku moja? Au kweli taifa litazaliwa kwa wakati mmoja?” (Isaya 66:8, NW) Katika 1919, watu wa Yehova walikuwapo tena wakiwa taifa la kiroho katika “bara” lao wenyewe, au hali ya kiroho duniani.
10. Kuanzia 1919, Wakristo watiwa-mafuta wamekuwa wakifurahia baraka zipi katika “bara” lao?
10 Wakiwa salama katika bara hilo, Wakristo watiwa-mafuta walitumikia katika hekalu kubwa la kiroho la Yehova. Wao waliitwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” wakikubali daraka la kutunza mali za kidunia za Yesu, pendeleo ambalo wangali wanafurahia karne ya 20 ikaribiapo mwisho. (Mathayo 24:45-47) Walijifunza vema somo la kwamba Yehova ndiye “Mungu wa amani mwenyewe.”—1 Wathesalonike 5:23.
11. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wamejionyeshaje kuwa maadui wa watu wa Mungu?
11 Lakini, namna gani juu ya maadui wa Israeli wa Mungu? Bidii ya Yehova kwa ajili ya watu wake yalingana na ghadhabu yake dhidi ya wapinzani. Wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walileta mkazo mkubwa sana walipojaribu—na kushindwa—kuondoa kabisa kikundi hiki kidogo cha Wakristo wenye kusema kweli. Wakati wa vita ya ulimwengu ya pili, wahudumu wa Jumuiya ya Wakristo waliungana katika jambo moja tu: Katika pande zote mbili zilizokuwa zikipambana, walihimiza serikali ziwakandamize Mashahidi wa Yehova. Hata leo, katika nchi nyingi viongozi wa kidini wanachochea serikali mbalimbali kuwekea vikwazo au kupiga marufuku kazi ya Kikristo ya kuhubiri ya Mashahidi wa Yehova.
12, 13. Ghadhabu ya Yehova yaonyeshwaje dhidi ya Jumuiya ya Wakristo?
12 Hilo halijakosa kuonwa na Yehova. Baada ya vita ya ulimwengu ya kwanza, Jumuiya ya Wakristo, pamoja na sehemu iliyobaki ya Babiloni Mkubwa, ilianguka. (Ufunuo 14:8) Uhalisi wa kuanguka kwa Jumuiya ya Wakristo ukaja kuwa jambo la kujulikana kwa wote wakati, kuanzia 1922, mfululizo wa mapigo ya mifano yalipomwagwa, yakifunua peupe hali yake ya kufa kiroho na kuonya juu ya uharibifu wake unaokuja. (Ufunuo 8:7–9:21) Huku kukiwa na uthibitisho kwamba kumwagwa kwa mapigo hayo kwaendelea, hotuba “Mwisho wa Dini Bandia U Karibu” ilitolewa ulimwenguni pote katika Aprili 23, 1995, ikifuatwa na kugawanywa kwa mamia ya mamilioni ya nakala za toleo la kipekee la Habari za Ufalme.
13 Leo, Jumuiya ya Wakristo iko katika hali ya kusikitisha. Kotekote katika karne ya 20, washiriki wayo wameuana katika vita vikatili vilivyobarikiwa na makasisi na wahudumu wayo. Haina uvutano wowote katika nchi fulani. Inaelekea kuharibiwa pamoja na sehemu inayobaki ya Babiloni Mkubwa.—Ufunuo 18:21.
-