Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Penda Kweli na Amani’!
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Januari 1
    • Kwa maana itakuwako mbegu ya amani; mzabibu utatoa matunda yake, nayo ardhi itatoa mazao yake, na hizo mbingu zitatoa umande wake; nami nitawarithisha mabaki ya watu hawa vitu hivi vyote.

  • ‘Penda Kweli na Amani’!
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Januari 1
    • (Zekaria 8:11-13) Ikiwa Israeli lingetenda kwa kuazimia, lingefanikiwa.

  • ‘Penda Kweli na Amani’!
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Januari 1
    • 7. (a) Ni mabadiliko gani yenye kusisimua ambayo watu wa Yehova wamepata, yakifikia upeo katika mwaka wa utumishi wa 1995? (b) Kwa kutazama ripoti ya kila mwaka, ni nchi zipi unazoona kuwa zina rekodi ya kutokeza ya wahubiri, mapainia, na wastani wa saa?

      7 Namna gani leo? Katika miaka ya kabla ya 1919, kwa njia fulani watu wa Yehova hawakuwa na bidii. Hawakuchukua msimamo thabiti wa kutokuwamo katika vita ya ulimwengu ya kwanza, nao walikuwa na mwelekeo wa kufuata mwanadamu badala ya Mfalme wao, Yesu Kristo. Tokeo likawa kwamba wengine walivunjwa moyo na upinzani kutoka ndani na nje ya tengenezo. Kisha, katika 1919, wakiwa na msaada wa Yehova wao waliacha mikono yao iwe hodari. (Zekaria 4:6) Yehova aliwapa amani, nao walisitawi sana. Hilo laonekana katika rekodi yao ya miaka 75 ambayo imepita, ifikiayo upeo katika mwaka wa utumishi wa 1995. Wakiwa kikundi, Mashahidi wa Yehova huepuka utukuzo wa taifa, ukabila, upendeleo, na vyanzo vingine vyote vya chuki. (1 Yohana 3:14-18) Wao humtumikia Yehova kwa bidii ya kweli katika hekalu lake la kiroho. (Waebrania 13:15; Ufunuo 7:15) Mwaka uliopita pekee, walitumia zaidi ya muda wa saa bilioni moja wakizungumza na wengine kuhusu Baba yao wa kimbingu! Kila mwezi, waliongoza mafunzo ya Biblia 4,865,060. Wastani wa 663,521 walishiriki katika utumishi wa painia. Wahudumu wa Jumuiya ya Wakristo watakapo kutoa kielelezo cha watu ambao kwa kweli ni wenye shauku katika ibada yao, nyakati nyingine wao hutaja Mashahidi wa Yehova.

      8. Kila Mkristo aweza kunufaikaje na “mbegu ya amani”?

      8 Kwa sababu ya bidii yao, Yehova huwapa watu wake “mbegu ya amani.” Kila mtu asitawishaye mbegu hiyo ataona amani ikikua moyoni mwake na maishani mwake. Kila Mkristo anayeamini ambaye hufuata amani pamoja na Yehova na pamoja na Wakristo wenzake hushiriki kweli na amani ya watu waitwao kwa jina la Yehova. (1 Petro 3:11; linganisha Yakobo 3:18.) Je, hiyo si ajabu?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki