-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Itakuwa siku hizo kwamba wanaume [wasio Wayahudi] kumi kutoka lugha zote za mataifa watashika, ndiyo, hakika watashika rinda la mwanamume aliye Myahudi, wakisema: ‘Sisi tutaenda na nyinyi watu, kwa maana sisi tumesikia kwamba Mungu yu pamoja na nyinyi watu.’” (Zekaria 8:23, NW)
-
-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
14. Ni jinsi gani Isaya 49:23 na Zekaria 8:23 yamekuwa na utimizo wa maana katika nyakati za ki-siku-hizi?
14 Katika nyakati za ki-siku-hizi, unabii kama vile Isaya 49:23 na Zekaria 8:23 umekuwa na utimizo wenye umaana sana. Likiwa tokeo la kuhubiri kwa jamii ya Yohana, hesabu kubwa za watu zimepitia ule mlango uliofunguliwa wakaingia ndani ya utumishi wa Ufalme.b Walio wengi wa hawa wametoka katika Jumuiya ya Wakristo, ambayo dini zayo hudai kwa ubandia kuwa Waisraeli wa kiroho. (Linga Warumi 9:6.) Hawa, wakiwa umati mkubwa, wanafua mavazi yao na kuyafanya meupe kwa kutumia imani katika damu ya dhabihu ya Yesu. (Ufunuo 7:9, 10, 14) Kwa kutii utawala wa Kristo wa Ufalme, wanatumaini kurithi baraka zao hapa duniani. Wanakuja kwa ndugu za Yesu wapakwa-mafuta na ‘kuwainamia,’ kiroho, kwa sababu ‘wamesikia kwamba Mungu yu pamoja nao.’ Wanahudumia hawa wapakwa-mafuta, ambao pamoja nao wanakuwa wenye umoja katika ushirika wa ndugu ulimwenguni pote.—Mathayo 25:34-40; 1 Petro 5:9.
-