Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mimi Nipo Pamoja Nanyi”
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Aprili 15
    • 20. Roho takatifu iliwasaidiaje Wayahudi kufanya mapenzi ya Mungu?

      20 Kulikuwa na upinzani mwingi uliokuwa kama mlima kutoka kwa maofisa wa serikali ambao walipiga marufuku kazi ya ujenzi. Hata hivyo, Yehova aliahidi kwamba “mlima” huo ungeondolewa na kuwa “nchi tambarare.” (Zekaria 4:7) Hivyo ndivyo ilivyokuwa! Mfalme Dario wa Kwanza alifanya uchunguzi, naye akagundua hati ya Koreshi ya kumbukumbu, ambayo iliwaruhusu Wayahudi kujenga upya hekalu. Basi, Dario akaondoa marufuku hayo, naye akaamuru kwamba Wayahudi wapewe pesa kutoka katika hazina ya kifalme ili kulipia gharama za ujenzi. Hilo lilikuwa badiliko lililoje! Je, roho ya Mungu ilihusika? Bila shaka. Ujenzi wa hekalu ulikamilishwa mwaka wa 515 K.W.K., katika mwaka wa sita wa utawala wa Dario wa Kwanza. —Ezra 6:1, 15.

  • Mikono Yenu na Iwe na Nguvu
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Aprili 15
    • 5, 6. Andiko la Zekaria 4:7 linatabiri utimizo wa jambo gani muhimu?

      5 Tuna uhakika kwamba kazi ya kuhubiri na kufundisha inayofanywa na watumishi wa Yehova watiifu wa wakati wetu itaendelea kwa msaada wake. Tunasoma hivi kwenye Zekaria 4:7: “Ataleta jiwe la juu kabisa. Nalo litapaaziwa sauti: ‘Linavutia kama nini! Linavutia kama nini!’” Unabii huo unahusu jambo gani muhimu ambalo limetimizwa katika siku zetu?

      6 Andiko la Zekaria 4:7 linatabiri wakati ambapo ibada ya kweli ya Bwana Mwenye Enzi Kuu ingefanywa kuwa kamilifu katika ua wa kidunia wa hekalu lake la kiroho. Hekalu hilo ni mpango wa Yehova wa kumfikia katika ibada kwa msingi wa dhabihu ya upatanisho ya Kristo Yesu. Ni kweli kwamba hekalu hilo kubwa la kiroho limekuwapo tangu karne ya kwanza W.K. Hata hivyo, bado ibada ya kweli duniani haijafanywa kuwa kamilifu. Sasa mamilioni ya waabudu wanatumikia katika ua wa kidunia wa hekalu hilo la kiroho. Watu hao pamoja na umati wa wale watakaofufuliwa watafanywa kuwa wakamilifu wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu Kristo. Mwishoni mwa hiyo miaka elfu, ni waabudu wa kweli wa Mungu tu ndio watakaobaki katika dunia iliyosafishwa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki