-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
14. (a) Ni nini kilichoonyeshwa na njozi ya Zekaria ya mizeituni miwili? na kinara cha taa? (b) Wakristo wapakwa-mafuta wangepatwa na nini wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu?
14 Zekaria aliishi wakati wa kujenga upya, na njozi yake ya mizeituni miwili ilimaanisha kwamba Zerubabeli na Yoshua wangebarikiwa kwa roho ya Yehova katika kuimarisha watu kwa ajili ya kazi. Njozi ya vinara vya taa ilikumbusha Zekaria ‘asidharau siku ya vitu vidogo’ kwa sababu makusudi ya Yehova yangetimizwa—“‘si kwa kani ya kijeshi, wala kwa nguvu, bali kwa roho yangu,’ Yehova wa majeshi amesema.” (Zekaria 4:6, 10; 8:9, NW) Kile kikosi kidogo cha Wakristo kilichodumu katika kupelekea aina ya binadamu nuru ya ukweli wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu kingetumiwa jinsi iyo hiyo katika kazi ya kujenga upya. Wao pia wangekuwa chanzo cha kitia-moyo na, wajapokuwa wachache, wangejifunza kutegemea imara ya Yehova, wasidharau siku ya mianzo midogo.
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 165]
Kazi ya Zerubabeli na Yoshua ya kujenga upya ilionyesha kwamba katika siku ya Bwana mianzo midogo ingefuatwa na ongezeko kubwa miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Imekuwa lazima kupanua sana vifaa kama hivi vinavyoonyeshwa juu, vilivyoko Brooklyn, New York, ili kusaidia kukidhi mahitaji yao
-