-
Yehova Huchukia Mwenendo wa HilaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
-
-
Wanaume hao walikuwa wakiwataliki wake zao kwa sababu mbalimbali zisizo na msingi, wakiwaacha wake wa ujana wao isivyofaa, labda ili waoe wanawake wachanga zaidi au wanawake wapagani. Nao makuhani wafisadi waliruhusu jambo hilo! Hata hivyo, andiko la Malaki 2:16 linasema: “Nakuchukia kuachana, asema BWANA, Mungu wa Israeli.” Baadaye, Yesu alionyesha kwamba msingi pekee wa talaka ambao ungefanya mwenzi asiye na hatia awe huru kufunga ndoa, ni uasherati.—Mathayo 19:9.
-
-
Yehova Huchukia Mwenendo wa HilaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 1
-
-
18. Unabii wa Malaki kuhusu hila unatuhusuje leo?
18 Bila shaka, shauri hilo kuhusu masuala hayo linatuhusu leo. Ni jambo la kusikitisha kwamba watu fulani hupuuza mwongozo wa Mungu wa kufunga ndoa katika Bwana tu. Pia inasikitisha kwamba wengine hukosa kujitahidi kuimarisha ndoa yao. Badala yake, wao hutoa udhuru na kufuata mwenendo unaochukiwa na Mungu kwa kuwapa wenzi wao talaka zisizo za Kimaandiko ili kufunga ndoa na mtu mwingine.
-