Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Tukutanike Pamoja?
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 15
    • Mathayo 11:28-30.

  • Kwa Nini Tukutanike Pamoja?
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 15
    • Chukueni nira yangu na mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mwenye tabia-pole na mnyenyekevu moyoni, nanyi mtapata burudisho kwa ajili ya nafsi zenu. Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”

  • Kwa Nini Tukutanike Pamoja?
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 15
    • “Nira Yangu Ni Laini na Mzigo Wangu Ni Mwepesi”

      Ona kwamba katika mistari tunayochanganua, Yesu alisema: “Mjifunze kutoka kwangu.” Kwa kujifunza kutoka kwa Yesu, tunakuwa wanafunzi wake, na tunachukua nira yake wakati tunapojiweka wakfu kwa Mungu na kubatizwa. (Mathayo 28:19, 20) Ili tuendelee kuwa wanafunzi wa Yesu ni muhimu tushiriki kwa ukawaida katika mikutano. Kwa nini? Kwa sababu, katika mikutano ya Kikristo tunafundishwa kumhusu Yesu, mafundisho yake, na njia zake.

      Kristo anataka tubebe mzigo gani? Ni mzigo uleule ambao yeye anabeba, yaani, pendeleo la kufanya mapenzi ya Mungu. (Yohana 4:34; 15:8) Jitihada inahitajiwa ili kutii amri za Mungu, lakini mzigo huo si mzito sana hivi kwamba hatuwezi kuubeba. Huenda ukaonekana kuwa mzito ikiwa tunajaribu kuubeba kwa nguvu zetu wenyewe. Hata hivyo, tukisali tupewe roho ya Mungu na tukila chakula cha kiroho kinachoandaliwa mikutanoni, tutapata “nguvu zinazopita zile za kawaida” ambazo zinatoka kwa Mungu. (2 Wakorintho 4:7) Kwa kujitayarisha kwa ajili ya mikutano na kushiriki katika mikutano, upendo wetu kwa Yehova unakuwa wenye nguvu hata zaidi. Na tunapochochewa na upendo, amri za Mungu haziwi “mzigo mzito.”—1 Yohana 5:3.

      Watu kwa ujumla wana matatizo mbalimbali kama vile matatizo ya kutafuta riziki, ya kiafya, na ya kibinafsi. Hata hivyo, hatutegemei hekima ya wanadamu tunapopambana na matatizo hayo. Mikutano ya kutaniko inatusaidia ‘kuacha kuhangaika,’ kwa kuwa Yehova anatosheleza mahitaji yetu naye anatusaidia kupambana na matatizo. (Mathayo 6:25-33) Bila shaka, mikutano ya Kikristo inaonyesha kwamba Mungu anatupenda.

      “Mimi Ni Mwenye Tabia-Pole na Mnyenyekevu Moyoni”

      Yesu alikuwa na desturi ya kwenda kwenye masinagogi, mahali ambapo Neno la Mungu lilizungumziwa. Pindi moja alipokuwa hekaluni, Yesu alichukua kitabu cha kukunjwa cha Isaya na kusoma hivi: “Roho ya Yehova iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuwatangazia maskini habari njema, alinituma kuhubiri kuachiliwa huru kwa mateka na kupata kuona tena kwa vipofu, kuacha waliopondeka waende zao wakiwa wameachiliwa huru, kuhubiri mwaka wa Yehova wenye kukubalika.” (Luka 4:16, 18, 19) Ingekuwa shangwe kama nini kumsikia Yesu akionyesha jinsi maneno hayo yalivyotimia aliposema: “Leo andiko hili ambalo mmesikia sasa hivi limetimizwa”!—Luka 4:21.

      Bado Yesu, “mchungaji mkuu” mwenye tabia-pole, anasimamia uchungaji wa kiroho wa wafuasi wake. (1 Petro 5:1-4) Chini ya mwelekezo wake, “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ameweka rasmi wanaume wawe wachungaji katika makutaniko ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. (Mathayo 24:45-47; Tito 1:5-9) Wanaume hao ‘wanalichunga kundi la Mungu’ kwa upole, nao wanaweka mfano mzuri kwa kuhudhuria mikutano kwa ukawaida. Unaweza kuonyesha kwamba unawathamini wanaume hao walio “zawadi katika wanadamu,” kwa kuhudhuria mikutano kwa ukawaida. Utawatia moyo wengine kwa kuwapo katika mikutano na kwa kushiriki.—Matendo 15:30-33; 20:28; Waefeso 4:8, 11, 12.

      “Mtapata Burudisho kwa Ajili ya Nafsi Zenu”

      Unapohudhuria mikutano ya Kikristo, unaweza kufanya nini ili pindi hizo ziwe zenye kuburudisha kwelikweli? Njia moja ni kufuata shauri hili la Yesu: ‘Kazia uangalifu jinsi unavyosikiliza.’ (Luka 8:18) Watu ambao kwa kweli walitaka kujifunza walimsikiliza Yesu kwa makini. Walimwomba afafanue mifano aliyotoa na, kwa sababu hiyo, walithawabishwa kwa kupewa uelewaji wenye kina zaidi.—Mathayo 13:10-16.

      Unaweza kuwaiga watu hao waliokuwa na njaa ya kiroho kwa kusikiliza kwa makini hotuba zinazotolewa katika mikutano yetu. (Mathayo 5:3, 6) Ili akili zako zisitange-tange, jitahidi kufuata hoja mbalimbali za msemaji. Jiulize maswali kama haya akilini mwako: ‘Ninaweza kutumia habari hii jinsi gani maishani mwangu? Ninaweza kuitumia kwa njia gani kuwasaidia wengine? Ninaweza kueleza jambo hili namna gani?’ Kwa kuongezea, fungua maandiko ambayo msemaji anatumia kuunga mkono mambo makuu. Kadiri unavyosikiliza ndivyo mikutano itakavyokuwa yenye kuburudisha zaidi.

      Baada ya mkutano, zungumza pamoja na wengine mambo yaliyozungumziwa mikutanoni. Fikiria habari hiyo na jinsi inavyoweza kutumiwa. Mazungumzo yenye kujenga yanafanya mikutano iwe yenye kuburudisha sana.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki