-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
Watu wakiwa wamelala usingizi, adui yake alikuja na kupanda magugu katikati ya ngano, naye akaondoka.
-
-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
5. Adui anayetajwa katika mfano huo ni nani, na magugu yanafananisha nani?
5 Adui ni nani, na magugu ni nani? Yesu anatuambia kwamba adui “ni Ibilisi.” Biblia inasema magugu ni “wana wa yule mwovu.” (Mt. 13:25, 38, 39) Kwa njia halisi, magugu ambayo Yesu alizungumzia huenda yalikuwa magugu fulani yenye sumu ambayo yanafanana sana na ngano ambayo haijakomaa. Mfano huo unawafaa sana Wakristo wa uwongo, wale wanaodai kuwa wana wa Ufalme lakini hawazai matunda yanayofaa! Wakristo hao wenye unafiki ambao wanadai kuwa wafuasi wa kweli wa Kristo kwa kweli wao ni sehemu ya “mbegu” ya Shetani Ibilisi.—Mwa. 3:15.
6. Magugu yalianza kutokea wakati gani, na watu walikuwa “wamelala usingizi” jinsi gani wakati huo?
6 Wakristo hao ambao ni kama magugu walitokea wakati gani? Yesu anasema hivi: “Watu wakiwa wamelala usingizi.” (Mt. 13:25) Ni wakati gani huo? Tunapata jibu katika maneno ambayo mtume Paulo aliwaambia wazee wa huko Efeso: “Ninajua kwamba baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wenye kukandamiza wataingia katikati yenu nao hawatalitendea kundi kwa wororo, na kutoka katikati yenu ninyi wenyewe watu watasimama na kusema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.” (Mdo. 20:29, 30) Kisha akawahimiza wazee hao wakae macho kiroho. Mitume, ambao walikuwa kama “kizuizi” kwa uasi-imani, walipoanza kulala usingizi katika kifo, Wakristo wengi walilala usingizi wa kiroho. (Soma 2 Wathesalonike 2:3, 6-8.) Uasi-imani mkubwa ulianza wakati huo.
7. Je, ngano iligeuka na kuwa magugu? Eleza.
7 Yesu hakusema kwamba ngano ingegeuka na kuwa magugu, alisema kwamba magugu yangepandwa katikati ya ngano. Kwa hiyo, mfano huo haumaanishi kwamba Wakristo wa kweli wangeacha kweli. Badala yake, unaonyesha kwamba Shetani angejitahidi kwa makusudi kulipotosha kutaniko la Kikristo kwa kuingiza watu waovu ndani yake. Mtume wa mwisho, Yohana, alipokuwa amezeeka, uasi-imani huo ulikuwa unaonekana waziwazi.—2 Pet. 2:1-3; 1 Yoh. 2:18.
-