-
Yehova Hutaka Nini Kutoka Kwetu Leo?Mnara wa Mlinzi—1999 | Septemba 15
-
-
“Huyu ni Mwana wangu, mpendwa, ambaye mimi nimemkubali; msikilizeni yeye.” (Mathayo 17:1-5) Kwa ujumla, Yehova hutaka haya kutoka kwetu—kumsikiliza Mwana wake na kufuata kielelezo na mafundisho yake. (Mathayo 16:24)
-
-
Yehova Hutaka Nini Kutoka Kwetu Leo?Mnara wa Mlinzi—1999 | Septemba 15
-
-
5. Wakristo wako chini ya sheria gani, na sheria hiyo ilianza kutenda lini?
5 Kumsikiliza na kumwiga Yesu kwahusisha nini? Je, kwamaanisha kuwa chini ya sheria? Paulo aliandika hivi: “Mimi mwenyewe siko chini ya sheria.” Alikuwa akirejezea “agano la zamani,” agano la Sheria lililofanywa na Israeli. Paulo alikiri kwamba yupo “chini ya sheria kuelekea Kristo.” (1 Wakorintho 9:20, 21; 2 Wakorintho 3:14) Agano la Sheria la zamani lilipokoma, “agano jipya” likaanza kutenda likiwa na “sheria [yake] ya Kristo” ambayo watumishi wote wa Yehova leo huwajibika kuitii.—Luka 22:20; Wagalatia 6:2; Waebrania 8:7-13.
-